-
Alivumilia Hadi MwishoIgeni Imani Yao
-
-
Akiwa ameazimia kulipiza kisasi, Ahazia akatuma kikosi cha askari 50 na mkuu wao waende kumkamata Eliya. Walipomkuta Eliya akiwa “ameketi kwenye kilele cha mlima,”a mkuu huyo wa jeshi akamwamrisha Eliya ‘ashuke chini’ katika jina la mfalme—jambo ambalo huenda lilimaanisha anaenda kuuawa. Wazia hilo! Hata ingawa askari hao walijua kwamba Eliya alikuwa “mtu wa Mungu wa kweli,” walifikiri eti wanaweza tu kumtisha. Walikuwa wamekosea kama nini! Eliya alimwambia hivi huyo mkuu: “Ikiwa kwa kweli mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni, ukuteketeze wewe na wanaume wako 50.” Kisha Mungu akatenda! “Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza pamoja na wanaume wake 50.” (2 Wafalme 1:9, 10) Msiba uliowapata askari hao ni kikumbusho cha wazi kwamba Yehova haoni kuwa ni jambo dogo kuwatendea watumishi wake kwa dharau au bila heshima.—1 Mambo ya Nyakati 16:21, 22.
-
-
Alivumilia Hadi MwishoIgeni Imani Yao
-
-
Eliya aliwezaje kuvumilia licha ya kuzungukwa na watu wakaidi? Hilo ni swali muhimu kwetu leo, sivyo? Je, umewahi kukasirika kwa sababu mtu fulani unayempenda alikataa kusikiliza maneno yenye hekima na kusisitiza afuate mwenendo wenye kudhuru? Tunawezaje kuvumilia hali kama hizo zenye kuvunja moyo? Tunaweza kujifunza jambo fulani kutokana na mahali ambapo askari walimkuta Eliya, yaani, “kwenye kilele cha mlima.” Hatuwezi kusema kihususa kwa nini Eliya alikuwa huko juu, lakini tunaweza kusema kwa uhakika kwamba kwa kuwa alikuwa na kawaida ya kusali, Eliya aliona kwamba eneo hilo lisilo na watu lilimpa nafasi nzuri ya kumkaribia zaidi Mungu wake aliyempenda. (Yakobo 5:16-18) Sisi pia tunaweza kutenga wakati wa kuwa peke yetu pamoja na Mungu, kusali kwake tukiliitia jina lake na kumweleza matatizo na wasiwasi tunaokabili. Tukifanya hivyo, itakuwa rahisi zaidi kuvumilia wakati watu wanaotuzunguka wanapotenda kwa njia zisizofaa na zinazowadhuru.
-
-
Alivumilia Hadi MwishoIgeni Imani Yao
-
-
a Wasomi fulani wamesema kwamba mlima unaotajwa hapa ni Mlima Karmeli, ambapo Mungu alimwezesha Eliya kuwashinda manabii wa Baali miaka michache mapema. Hata hivyo, Biblia haisemi waziwazi ulikuwa mlima gani.
-