-
‘Tunajua Watainuka Katika Ufufuo’Mnara wa Mlinzi—1989 | Juni 15
-
-
‘Ebu ngoja kidogo,’ huenda watu fulani wanaojua kidogo habari za Biblia wakakinza, ‘kwani Ayubu hakusema katika sura ya Ayubu 16, mstari 22, kwamba ‘angeenda’ kwa kufuata ‘njia ambayo hangerudi tena’? Na kwenye Ayubu 7:9, NW, alionyesha wazi hivi: “Yeye anayeenda chini Sheoli [kaburini] hatakuja juu.” Ayubu aliongezea hivi katika Ayubu 7 mstari wa 10: “Yeye hatarudi tena kamwe kwenye nyumba yake, na mahali pake hapatamkiri tena kamwe.’”
Kwa hiyo, kama wanavyodai wanachuo fulani, je! mistari hiyo na taarifa zinazofanana nayo haionyeshi kwamba Ayubu alikiona kifo kuwa ‘bara linaloendewa bila kurudi’? Je! taarifa hizo zinamaanisha kwamba Ayubu hakuamini katika ufufuo wa wakati ujao? Ili kupata jibu, ni lazima tuchukue maneno haya kulingana na habari zinazohusika, pia kuyalinganisha na mawazo mengine ambayo Ayubu alieleza kuhusu habari hiyo.
Ayubu hakujua sababu za kuteseka kwake. Kwa muda fulani alikosea kufikiri kwamba Mungu ndiye aliyekuwa akileta dhiki yake. (Ayubu 6:4; 7:17-20; 16:11-13) Kwa kuvunjika roho, yeye alihisi kwamba mahali ambapo angepata kitulizo cha mara hiyo pangekuwa ni kaburini tu. (Ayubu 7:21; 17:1; linganisha 3:11-13.) Akiwa huko, kulingana na maoni ya marika wake, hangeonwa, hangerudi kwenye nyumba yake, hangezidi kutambuliwa, hangerudi wala hangekuwa na tazamio lolote la kufanya hivyo kabla ya wakati wa Mungu uliowekwa. Ayubu na wazao wengine wote wa Adamu hawakuwa na nguvu za kuinuka kutoka kwa wafu wakiachiliwa peke yao bila hatua kuchukuliwa na Mungua—Ayubu 7:9, 10; 10:21; 14:12.
-
-
‘Tunajua Watainuka Katika Ufufuo’Mnara wa Mlinzi—1989 | Juni 15
-
-
a Kuhusu wazo ilo hilo, mtunga zaburi anaandika hivi juu ya hali iliyopo wakati huo kabla ya Mungu kuchukua hatua yoyote: “Na [Mungu] akaendelea kukumbuka kwamba [Waisraeli] walikuwa mnofu, kwamba roho [au kani ya uhai kutoka kwa Mungu] inaenda ikitokeza mbele na hairudi.”—Zaburi 78:39, NW.
-