Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 5/15 kur. 26-29
  • Bara la Ndege Kipilipili Lausikia “Wimbo Mpya”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Bara la Ndege Kipilipili Lausikia “Wimbo Mpya”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • “Wimbo Mpya” Wafika Liberia
  • Itikio kwa “Wimbo Mpya” Leo
  • “Wimbo Mpya” Wafikia Kilele
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 5/15 kur. 26-29

Bara la Ndege Kipilipili Lausikia “Wimbo Mpya”

KUNAPOPAMBAZUKA, sauti yenye madoido mazuri ya ndege kipilipili husikiwa kote kote katika Liberia. Kwa vizazi vingi, udoido wa sauti yake umetumika kuamsha wanavijiji waamkie siku nyingine ya kazi chini ya jua la kitropiki. Ndege huyu anayeimba mahali pengi ameipa nchi ya Liberia jina layo la kubandikwa, “bara la ndege kipilipili.”

Hata hivyo, jina Liberia linaleta akilini hadithi nyingine. Katika 1822 watumwa wakombolewa wenye kurudi kutoka Amerika kuja kwenye kontinenti ya baba zao watangulizi waliwasili kwenye kinywa cha Mto Mesurado na kufanyiza eneo la ulowezi lililokuja kuwa Monrovia. Maeneo mengine ya ulowezi yalisitawi Buchanan, Greenville, na Harper, na walowezi wakafanya mikataba pamoja na wafalme wa makabila ya wenyeji. Wenye kurudi mapema hiyo walikuja wakiwa na tenzi za kiroho za Waamerika-weusi​—nyimbo zilizounganisha midundo ya Kiafrika na mawazo ya Kibiblia na kuonyesha walivyotamani sana kupata uhuru. Kwa kupatana na tamanio hilo, katika 1824 koloni lao liliitwa Liberia. Katika 1847 likawa ndiyo jamhuri ya kwanza ya weusi katika Afrika.

Hata hivyo, katika miaka ya majuzi wimbo mpya umesikiwa katika bara hili. Huu ni wimbo unaoimbwa, si na ndege kipilipili wala na watumwa waliorudishwa, bali na korasi inayoongezeka ya watu wanaoitikia himizo la mtunga zaburi wa Kibiblia: “Mwimbieni BWANA [Yehova, NW] wimbo mpya, mwimbieni Bwana [Yehova, NW], nchi yote. Semeni katika mataifa, Bwana [Yehova, NW] ametamalaki.” (Zaburi 96:1, 10) Ndiyo, huu ndio wimbo wa Ufalme wa Mungu uliosimamishwa imara, Yesu Kristo akiwa ndiye Mfalme. Unaimbwa na wanaotazamiwa kuwa warithi wa serikali ya kimbingu ya Yehova. Wao na waandamani wao wanapiga kwa shangwe mbiu ya “habari njema” zinazohusu Ufalme huo katika mataifa yote​—kutia ndani Liberia​—wakati wa “umalizio wa mfumo wa mambo,” ambamo sisi sasa tunaishi. (Mathayo 24:3, 14, NW) Ni wakati gani na jinsi gani wimbo huu ulivyopata kusikiwa kwanza katika bara la ndege kipilipili? Na melodia yao yenye kupekua mioyo imekuwa na matokeo gani juu ya wasikiaji wenye uthamini? Acheni tusikilize.

“Wimbo Mpya” Wafika Liberia

Katika 1946 Harry C. Behannan, mweusi mwenye kipawa cha kupiga piano aliyekuwa amefanya maonyesho ya upigaji katika sehemu zote za Ulaya, aliacha kazi-maisha yake ya kimuziki ili atumikie akiwa misionari. Kwa miezi sita alitumikia peke yake akiwa Shahidi painia wa Yehova, akienda nyumba kwa nyumba kueneza ukweli wa Ufalme. Aliangusha vitabu zaidi ya 500 na kuwa rafiki ya watu wengi. Halafu ikawa ni tanzia Ndugu Behannan alipokufa kwa homa kali ya kitropiki. Lakini ule “wimbo mpya” haukufifilia mbali, kwa maana wamisionari wengine walimfuata.

Katika 1947 George Watkins (aliyekuwa mwanandondi asiyelipwa) na Willa Mae mkewe wakaja kutumikia katika Monrovia, mji mkuu wa Liberia. Walikuwa wenye saburi na bidii-endelevu katika kuwafundisha Waliberia wanyenyekevu ‘kushika mambo yote ambayo Yesu aliwaamuru.’ (Mathayo 28:19, 20, NW) Kufikia Septemba 1948 kikundi cha watu 15 kilikuwa kikishiriki pamoja nao katika utumishi wa Ufalme. Hivyo, kundi la kwanza la Mashahidi wa Yehova likafanyizwa katika Liberia.

Kazi ya kuhubiri ilienea kwa haraka sana kuteremka chini pwani hadi bandari ya Harper, katika Kakata na vijiji vyenye kuizunguka, na miongoni mwa wachanja mipira Wakisi kwenye shamba la Firestone. Kufikia 1952 ofisi ya tawi la Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi ilianzishwa katika Liberia. Mwaka uliofuata, Jumba la Ufalme la kwanza pamoja na kao la wamisionari lilijengwa katika McDonald Street katika Monrovia. Hizo zilikuwa nyakati za kusisimua. Leo, kuna wasifaji 1,724 wa Yehova katika bara hili, nao wanapata matokeo mazuri sana miongoni mwa watu hawa wenye urafiki, ukaribishaji, na unyenyekevu.

Itikio kwa “Wimbo Mpya” Leo

Mashahidi wa Yehova wa kutoka makabila yale 16 makubwa-makubwa ya Liberia, pamoja na wamisionari na watu mmoja mmoja ambao wamekuja kutumikia mahali ambapo uhitaji ni mkubwa zaidi, sasa wamechanganya sauti zao katika kuuvumisha ujumbe wa Ufalme. Juzijuzi, wameongezea uharaka katika kusihi wale wanaotafuta ukweli. Kwa wastani, kila Shahidi anatumia saa zaidi ya 27 kwa mwezi katika kazi ya kuhubiri, na hesabu ya wale walio katika huduma ya wakati wote imeongezeka zaidi ya mara tatu katika miaka mitano iliyopita. Jitihada hizo zimeleta mibaraka kwao na kwa wengine pia. Acheni tusikie baadhi ya mibaraka hiyo.

Emmanuel alirekebisha mambo yake ili aweze kutunza jamaa yake kubwa na kushiriki katika kazi ya painia wa wakati wote katika Gardnersville. Aliwakuta Varney na Lucinda na kuanza funzo la nyumbani la Biblia pamoja nao. Hata hivyo, wao waliamini kwamba ni dhambi mtu kubadili dini yake. Emmanuel aliwaonyesha kinavyosema kitabu Reasoning From the Scriptures juu ya habari hiyo. Walikiazima kitabu hicho, wakasoma habari zilizomo, na kuanza kuhudhuria mikutano ya Kikristo. Muda mfupi baadaye, walianza huduma ya Kikristo. Kwa sasa, mpangishaji wa nyumba waliyokaa​—kasisi​—aliona badiliko katika mwenendo wao na kuwaalika watumie chumba chake cha maongezi kwa ajili ya funzo lao la Biblia. Baada ya kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya, huyo mpangisha nyumba alisadiki kwamba alikuwa ameupata ukweli na akaomba funzo lake mwenyewe la Biblia.

Kuuitikia “wimbo mpya” kulimkomboa Tamba, mtu wa kutoka Lofa County ambaye alikuwa kipitio cha kuwasiliana na roho. Kwa kuingiwa na wasiwasi kuhusu ugonjwa wa mwana wake, alikuwa ameomba ushauri kutoka kwa roho. Wao wakamhakikishia kwamba mwana wake angeishi lakini wakadai kwamba mke wake alikuwa akipanga hila ili mwana wake afe. Kwa kutumia matoleo na dhabihu, Tamba akawasihi sana roho hao waue mke wake ili kumzuia kudhuru mwana wake. Tokeo likawa nini? Mwana huyo alikufa lakini mke akawa bila dhara. Kwa kukasirika na kuvurugika akili, Tamba alitupa nje vikorokoro vyake vyote vya kuwasiliana na roho hao. Katika hali yake ya kihoro, ujumbe unaohusu tumaini la ufufuo na dunia paradiso inayokuja ulimgusa kwa kina kirefu. Alikubali funzo la Biblia, akasafisha maisha yake, na kujiweka wakfu kwa Yehova. Tangu wakati huo amesaidia jamaa yake na watu wengine tisa katika mtaa wao wajiweke wakfu.

Maisha za wengi wenye mioyo ya ufuataji haki yaliguswa na ule “wimbo mpya.” Herbert alifaulu kutuzwa uanachuo kwenye chuo kikuu cha Monrovia na kazi ya serikali kwa sababu ya uhodari wa kucheza mpira. Hata hivyo, alipojifunza inavyosema Biblia kuhusu roho ya mashindano, alisukumwa na moyo kuacha kazi-maisha yake ya uchezaji. (Wagalatia 5:26) Sasa yeye anaona shangwe katika kazi-maisha yake mpya akiwa mhudumu wa wakati wote.

James alimuuliza Shahidi mwenye kujifunza naye jinsi angeweza kushinda uzoelevu wake wa kutumia bangi. Alipotiwa moyo asali kuhusu jambo hilo, James alimwomba Yehova amsaidie kuacha. Majuma kadhaa baadaye, alishindwa kuikinza ile tamaa kali na akavuta tena. Akiwa njiani kwenda nyumbani, alijigonga sana kwenye ufito wa chuma akatoka sana damu kandokando ya jicho lake. Kwa kukumbuka sala yake, hakulirudia kamwe zoea lake. Leo, yeye anatumikia akiwa painia wa kawaida na mtumishi wa huduma katika kundi.

Usihi wa ule “wimbo mpya” umefikia mwanamume mzee pia, Samuel wa kabila la Krahn, ambaye hapo zamani alikuwa msimamizi mkuu wa Montserrado County. Ni nini kilichomsukuma kuacha kazi-maisha yenye mshahara wa juu na kufuatia huduma ya wakati wote? “Kilichonivutia ni uhakika wa kwamba katika Biblia yangu ningeweza kupata jambo la kuunga mkono kila kitu ambacho Mashahidi wa Yehova walisema, wakafundisha, na kufanya,” akasema Samuel. Aliongezea kwamba ameupata miongoni mwa Mashahidi wa Yehova upendo ambao Yesu aliueleza kwenye Yohana 13:34, 35. Samuel aliona kwamba, kinyume cha hivyo, washiriki wa kanisa alilokuwa “walikuwa wakizozana sikuzote na kupigania mambo ya pesa mle mle kanisani.” Sasa Samuel anatumikia akiwa painia wa kawaida.

“Wimbo Mpya” Wafikia Kilele

Kwa habari ya kumwimbia Mungu sifa, hakuna nyakati zenye furaha zaidi kwa watu wa Yehova kuliko mikusanyiko yao ya wilaya ya kila mwaka. Hata hivyo, katika miaka ya majuzi, hapa katika Liberia tatizo limekuwa kupata sehemu zenye nafasi kubwa ya kuwatosha Mashahidi wote na watu wenye kupendezwa ambao wangehudhuria. Katika 1986 mikusanyiko miwili ilifanywa kwenye oditoriamu ile moja tu inayofaa, lakini hudhurio la ujumla la watu zaidi ya 4,000 liliilemea sehemu hiyo. Ni jambo gani lingefanywa kuhusu 1987? Basi, uwanja unaoitwa Samuel K. Doe Sports Complex ulimalizwa kwa wakati unaofaa kwa usaidizi wa serikali ya China. Lakini je! tungeweza kukodisha sehemu hii?

Kwa sababu programu yetu ilikuwa ya kielimu, wasimamizi walikubali tutumie stediamu hiyo kwa malipo mazuri sana. Lakini majuma machache tu kabla ya wakati wa mkusanyiko, wasimamizi hao wakataka kuongeza pesa walizotoza. Kwa nini? Kwa sababu ndiyo sasa tu mwevanjeli fulani mashuhuri wa televisheni kutoka United States alikuwa amemaliza shughuli yake ya kidini katika stediamu, na umati ulikuwa umeiacha ikiwa katika hali ya kusikitisha sana, takataka zikiwa zimetapakaa kila mahali. Wasimamizi hao walihakikishiwa kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa tofauti. Siku iliyotangulia mkusanyiko, ndugu na dada zaidi ya 500 waliisafisha stediamu kabisa. Baada ya mkusanyiko, mshiriki mmoja wa kikundi cha wasimamizi Wachina wa uwanja huo alisikiwa akisema kwamba jitihada yetu ya kutunza usafi wa stediamu ilistahili malipo mengi kuliko kiasi kile tulicholipa kuitumia.

Mkusanyiko wenyewe ulifanikiwa. Kilele kipya cha watu 5,852 walihudhuria hotuba ya watu wote “Katika Nyakati Hizi Zenye Hofu, Unaweza Kuitibari Nani?” Ilikuwa shangwe iliyoje kuona wapya 101 wakifananisha wakfu wao kwa Mungu kwa kuzamishwa katika maji! Mabatizo yalitukia katika vidimbwi viwili vyenye kubebeka kwenye uwanja wa mkusanyiko​—ulio wa kwanza kwa Liberia!

Kwa sababu ya watu wenye kuongezeka wanaoitikia ule “wimbo mpya,” ofisi ya kwanza ya tawi katika McDonald Street katika Monrovia ilikuwa imethibitika kuwa ndogo mno. Hata jengo lililofuata hilo katika Sinkor halikuwa na ukubwa wa kutosha kuweka akiba ya vitabu vyote vya Biblia vilivyohitajiwa kutimiza mahitaji ya kiroho ya Waliberia. Kwa hiyo, jengo kubwa la makao lilinunuliwa na kurekebishwa upya karibu na Jumba la Ufalme la Paynesville, na ofisi ya tawi iliyo mpya ikawekwa wakfu siku ya Machi 28, 1987. Wakiwa na jengo hili lenye nafasi kubwa na lililo mahali pazuri sana, watumishi wa Yehova katika Liberia wana vifaa vya kutosha kutunza upendezi ule unaoongezeka.

Ni kazi ya kiasi gani inayobakia kufanywa katika Liberia? Hudhurio la Ukumbusho wa 1988 la watu 8,600​—mara tano ya hesabu ya wahubiri wa Ufalme​—linaonyesha kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kutokea wanafunzi wengi zaidi. Na Mashahidi Waliberia wenye bidii wanaitikia wito huo wa ushindani. Wanaongoza mafunzo ya nyumbani ya Biblia zaidi ya 3,000 kila mwezi. Sala yetu ni kwamba wengi zaidi hapa wajiunge katika “umati mkubwa” unaoongezeka daima ambao wanamsifu Yehova kwa kuuitikia “wimbo mpya.”​—Ufunuo 7:9, 10.

[Sanduku katika ukurasa wa 28]

Kutoka Nyumba Hadi Nyumba Katika Liberia

Tunapokaribia nyumba ya mikongojo na matope, badala ya kupiga hodi, sisi hutangaza kuwapo kwetu kwa kuita hivi: “Kpaw, kpaw, kpaw!

Tusipopata jibu, tunatembea nyuma ya nyumba ile na kupata jamaa ikiwa imeketi “jikoni”​—kibanda kidogo katika ua wa nyuma. Nyungu yenye siagi nyekundu nzito ya mtende inachemka juu ya moto wa kuni. Mama, ambaye anapakua wali, anatuma watoto wake waharakishe nyumbani kutuletea viti.

Sasa washiriki wa jamaa wanatulia. Wakiwa wamekalia kiti cha ubao, wanasikiliza kwa makini tunapotokeza ujumbe wa UfaIme. Wanafurahi kukubali nakala ya broshua Furahia Milele Maisha Duniani! nasi tunafanya mipango ya kurudi. Tunapoinuka kwenda zetu, wanasema: “Tule kwanza!”

[Ramani/​Picha katika ukurasa wa 26]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

SIERRA LEONE

LIBERIA

LOFA COUNTY

MONTSERRADO COUNTY

Monrovia

Kakata

Buchanan

Greenville

Harper

GUINEA

IVORY COAST

ATLANTIC OCEAN

Km 0 100 200 300

mi 0 100 200

[Ramani]

AFRIKA

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki