Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 5/15 uku. 30
  • Muono-Ndani Juu ya Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Muono-Ndani Juu ya Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Mtazamo wa Pili”
  • Kupagawa Hatari
  • Hakuna Fumbo
  • Ninaweza kuepukaje Ponografia?
    Amkeni!—2007
  • Madhara Yanayosababishwa na Ponografia
    Amkeni!—2003
  • Kwa Nini Ujiepushe na Ponografia?
    Vijana Huuliza
  • Kwa Nini Niepuke Ponografia?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 5/15 uku. 30

Muono-Ndani Juu ya Habari

“Mtazamo wa Pili”

Mwanzo 1:1, ZSB, unataarifu hivi: “Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” Kwa zaidi ya karne moja, wanasayansi wanaopendelea nadharia ya mageuzi wamechambua mstari huu wa Biblia. Hata hivyo, “wengi wao sasa wanafanya mtazamo wa pili kuhusu ushuhuda huu wa mapema zaidi, ulio wenye nguvu zaidi kwamba kuna Muumba,” linaripoti The Orange County Register, gazeti la habari la Kalifornia.

Kwa kielelezo, makala hiyo inataarifu yale yanayosemwa na mwanabayolojia Mwaustralia Michael Denton katika kitabu chake Evolution: A Theory in Crisis. Yeye anashikilia kwamba tangu Darwin alipokitangaza kwa chapa kitabu chake On the Origin of Species mpaka sasa, hakujawa hata na kiushuhuda kidogo cha kuunga mkono nadharia ya Darwin.

Vivyo hivyo, Register inatoa kielelezo cha jambo hilo kwa kutaja kitabu The Mystery of Life’s Origins: Reassessing Current Theories, kilichoandikwa na wanasayansi watatu. Kulingana na gazeti hilo, wao wanaeleza kwamba maisha yasingaliweza kuwa yalianza kwa nasibu na “wanatoa hoja ya kwamba ‘Muumba [fulani] aliye mbele ya mipaka ya ulimwengu’ ndiye anayeweza kuelezeka kiakili kuwa chanzo cha uhai.” Ikiunga mkono maoni haya, makala hiyo inataja kwamba mchunguzi wa nyota Mwingereza Fred Hoyle “anatajwa mahali pengi sana kuwa alitaarifu kwamba kuamini chembe ya kwanza yenye uhai ilitokea kwa nasibu ni kama kuamini kwamba tufani yenye kupita kasi katika uwanja wa takataka uliojaa sehemu za ndege ingeweza kutokeza ndege ya muundo wa Boeing 747.”

Kwa wanasayansi kadhaa, ushuhuda wa kuunga mkono kwamba kuna Msababishi Mkuu Zaidi ni hakika kabisa. Hata hivyo, namna gani wale wanaozidi tu kukana kuwako kwa Muumba? Watu wa jinsi hiyo wangefaa kufikiria maneno haya yaliyoandikwa na mnabii Isaya: “Ninyi mnapindua mambo; Je! mfinyanzi ahesabiwe kuwa kama udongo; kitu kilichofinyangwa kimnene yeye aliyekifinyanga, Hakunifinyanga huyu?”​—Isaya 29:16.

Kupagawa Hatari

Katika Januari ya mwaka huu, muuaji wa mfululizo Theodore Robert Bundy, aliwekwa katika kiti cha nguvu za umeme katika Gereza la Florida State (United States, Amerika) na kuuawa. Alikuwa amehusika katika vifo vya ukatili vya kufikia wanawake 36, ingawa wenye mamlaka wanashuku kwamba tarakimu hiyo ingeweza kuwa juu kufikia 100.

Katika hoji moja kabla ya kuuawa kwake, Bundy alikiri kwamba vitabu vyenye picha za umalaya vilikuwa jambo kubwa Iililochangia mwenendo wake wa uhalifu. Kulingana na Dakt. James Dobson, aliyeendesha hoji hilo, “akiwa na miaka 12 au 13 yeye alianza kutafuta vitabu vyenye picha za umalaya katika maduka ya kuuzia dawa, hata kandokando ya barabara, naye akawa mzoelevu, mwenye kupagawa,” inaripoti Daily News.

Ungamo la Bundy linafanana na maneno ya Arthur Gary Bishop, aliyeuawa mwaka jana kwa mauaji yaliyohusu ngono ya wavulana watano. Kulingana na The Tribune, gazeti moja la habari la San Diego, Kalifornia, Bishop alikazania kwamba vitabu vyenye picha za umalaya ‘“vilimteketeza’ akiwa mvulana na kuongoza kwenye anguko lake.” Bishop alitaja maneno ya mwanasaikolojia aliyetoa ushuhuda kwenye kesi yake kwamba “watu wanapokuwa wazoelevu [wa vitabu vyenye picha za umalaya] tamaa zao zinaongezeka sana, hisia zao za kawaida zinakufa ganzi na wanaelekea kutenda mambo ambayo wameona.” Bishop aliungama hivi: “Ndivyo ilivyokuwa kuhusu mimi. Mimi ni mwanamume mlala-wavulana ambaye ameshtakiwa uuaji, na vitabu vyenye picha za umalaya vilihusika sana katika anguko langu.”

Hata ingawa wenye kuungama uuaji wao wamekiri kwamba vitabu vyenye picha za umalaya vina uharibifu, kuna watu wengi ambao wangali wakiviona kuwa utumbuizo usiodhuru. Hata hivyo, onyo lililotolewa kwenye Isaya 5:20 linatumika vizuri kwa watu hao: “Ole wao wasemao kwamba uovu ni wema, na kwamba wema ni uovu; watiao giza badala ya nuru, na nuru badala ya giza.”

Hakuna Fumbo

Mhudumu wa United Church Phyllis Smith anadai kwamba imani ya baadhi ya makasisi inaonekana kuwa ikitishwa na maswali ya watu walio na magonjwa yasiyotibika, inaripoti The Toronto Star, gazeti la habari la Kanada. Kulingana na Smith, “watu wenye kufa wanauliza maswali juu ya mafumbo ya uhai na kifo yasiyoeleweka na mtu yeyote.” Mwanamke huyo anasema: “Hatuhitaji kuhisi tunatishika kwa sababu tu tunahisi kwamba tunapaswa kuwa na majibu yote.” Wakati maswali magumu ya kiroho yanapotokezwa, Smith anashikilia kwamba makasisi “hawahitaji kumtetea Mungu.”

Ingawa ni kweli kwamba huenda watu mmoja mmoja wasiwe sikuzote na majibu yote kwa maswali yanayohusu uhai na kifo, Biblia inayo. Je! wale wanaodai kuwa wahudumu wa Mungu hawapaswi kujua Neno lake linasema nini? Mtume Petro alisema kwamba waamini wenzake wanapaswa kuwa “tayari sikuzote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu.” (1 Petro 3:15) Wakristo wa mapema hawakuwa na tatizo kuelewa hali ya wafu au matazamio ya wakati ujao ambayo yanatolewa kwa aina ya binadamu wenye kufa. Walijua kwamba Mhubiri 9:5 inasema hivi: “Walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote.” Na Yesu aliambia wafuasi wake hivi: “Saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” (Yohana 5:28, 29) Kwa wahudumu wa kweli wa Mungu, uhai na kifo hauna fumbo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki