-
Vielelezo vya Unyenyekevu vya KuigaMnara wa Mlinzi—1993 | Desemba 1
-
-
4. Ni maandiko gani huonyesha kwamba Yehova ni mnyenyekevu?
4 Yehova Mungu—aliye Juu Kabisa, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote Mzima, Mfalme wa umilele—ni mnyenyekevu. (Mwanzo 14:22) Je! hilo lawezekana? Bila shaka, ndiyo! Mfalme Daudi alisema, kama ilivyorekodiwa kwenye Zaburi 18:35: “Umenipa ngao ya wokovu wako, mkono wako wa kuume umenitegemeza, na unyenyekevu wako umenikuza.” Kwa wazi, Mfalme Daudi aliuona unyenyekevu wa Yehova kuwa ndiyo sababu ya kukuzwa kwake, Daudi. Kisha tena, twasoma kwenye Zaburi 113:6 kwamba Yehova ‘anyenyekea kutazama mbinguni na duniani.’ Tafsiri nyinginezo husoma, “ainama chini kutazama,” (New International Version) “ajidhili kutazama chini sana.”—The New English Bible.
5. Ni matukio gani ambayo hushuhudia unyenyekevu wa Yehova?
5 Kwa hakika Yehova Mungu alijinyenyekeza katika njia aliyoshughulika na Abrahamu, akimruhusu Abrahamu kumwuliza juu ya uadilifu Wake katika kukusudia kuharibu majiji maovu ya Sodoma na Gomora.(Mwanzo 18:23-32) Na Yehova alipoeleza nia yake ya kuharibu taifa la Israeli—wakati mmoja kwa sababu ya ibada ya sanamu, na wakati mwingine kwa sababu ya uasi—katika kila pindi Musa alisababu na Yehova kana kwamba alikuwa akiongea na binadamu mwingine. Kila mara Yehova aliitikia kwa kukubali. Kujibu sihi za Musa kwa niaba ya watu Wake Israeli kulionyesha unyenyekevu. (Kutoka 32:9-14; Hesabu 14:11-20) Vielelezo vingine vya Yehova akishughulika na wanadamu kwa unyenyekevu, kana kwamba mtu kwa mtu, vyaweza kuonwa katika mahusiano yake na Gideoni na Yona, kama yalivyorekodiwa kwenye Waamuzi 6:36-40 na Yona 4:9-11.
-