Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 11/1 uku. 5
  • “Kujibu kwa Njia ya Unyoofu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kujibu kwa Njia ya Unyoofu”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Kukaripia “Mbele ya Watazamaji Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Tembea Katika ‘Njia ya Unyofu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kutumia Biblia Kujibu Maswali
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Wazee, Hukumuni kwa Uadilifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 11/1 uku. 5

“Kujibu kwa Njia ya Unyoofu”

KATIKA Mahubiri ya Mlimani, Yesu alirejezea “torati na manabii.” Kisehemu cha tatu cha Maandiko ya Kiebrania kilikuwa ile Miandiko, ambayo ilitia ndani vitabu vya kishairi, kama vile Zaburi na Mithali. (Mathayo 7:12; Luka 24:44) Hivi, pia, vina hekima ya Mungu.

Kwa kielelezo, mithali ziliwaonya hivi mahakimu katika Israeli ya kale: “Yeye ambaye anasema hivi kwa mtu mwovu: ‘Wewe ni mwadilifu,’ jamii za watu zitamfanya kinyaa, vikundi vya kitaifa vitamkataa katakata. Lakini kwa wale wanaomkaripia litakuwa jambo la kufurahisha, na juu yao itakuja baraka ya wema. Yeye ambaye anajibu kwa njia ya unyoofu atabusu midomo.”—Mithali 24:24-26, NW.

Kama hakimu angejiacha ashindwe na mibano ya kuchukua hongo au kupendelea watu wa ukoo wake na kumtangaza mwovu kuwa mwadilifu, wengine wangeona hafai kuwa katika cheo chake. Kwani, hata washirika wa “vikundi vya kitaifa” vya watu Wasio Wayahudi wenye kusikia kuhusu kitendo hicho haramu wangedharau sana jambo hilo! Kwa upande ule mwingine, kama hakimu angemkaripia mtu mwovu kwa moyo mkuu na kuijibu kesi iliyopo kwa njia ya unyoofu, hapo angejipatia staha na upendo wa watu. Watu kwa ujumla wangesukumwa na mioyo yao kumtakia “baraka ya wema.” Kama vile mithali hiyo iendeleavyo kuliweka wazo lenyewe: “Yeye ambaye anajibu kwa njia ya unyoofu atabusu midomo.”

Busu la jinsi hilo lilionyesha staha ya pande mbili—kati ya mshauri na wale wanaoshika karipio lake la unyoofu. Labda hata mkaripiwa mwenyewe angeitikia kwa njia yenye kupendeleka na kumwonyesha shauku hakimu huyo. Yasema hivi Mithali 28:23, NW: “Yeye ambaye anakaripia mtu atapata upendeleo zaidi baadaye kuliko yeye ambaye anarairai kwa ulimi wake.” Kwa hiyo wale wanaotumikia wakiwa wazee wa kundi leo ni lazima waepuke kuruhusu urafiki au mahusiano ya kijamaa yapotoshe hukumu yao. Kwa kutoa kwa unyoofu shauri lenye kuhitajiwa, wazee watajipatia staha ya kundi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki