-
Maswali Wanayouliza Watu Juu ya KileoMnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
-
-
Wengine hata wanatoa hoja ya kupendelea kutokunywa hata kidogo. Kiongozi wa kidini wa Naijeria aliyetajwa hapo juu anadai hivi: “Mithali 20:1 inasema waziwazi kwamba wale wanaokunywa divai si wenye hekima.” Na bado mhubiri mwingine anadai kwa nguvu nyingi: “Maandiko Matakatifu yanalaumu vikali kileo katika Kitabu cha Isaya,” akirejeza kwenye maandiko kwenye Isaya 5:11, 12, na Isa 5:22.
-
-
Kileo Ni Nini Yaliyo Maoni ya Mkristo Juu Yacho?Mnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
-
-
“Hana Hekima”—Nani?
Je! hii inamaanisha kwamba kileo kinakatazwa kabisa kabisa kwa Wakristo? Namna gani juu ya lile dai la yule kiongozi wa kidini aliyetajwa katika makala iliyotangulia, linalodhaniwa kuwa msingi wake ni Mithali 20:1, kwamba “watu wenye hekima hawanywi divai kabisa.” Tafsiri ya Union Version hutafsiri mstari huu hivi: “[Divai, NW] hudhihaki, kileo huleta ugomvi; na akosaye [“anayedanganywa na,” KJ] kwa vitu hivyo hana hekima.” Tena, Biblia haiwaadhibu wale ambao hunywa divai, bali, badala yake, wale ambao hudanganywa nayo! “Wale wakaao sana kwenye [divai, NW]” na “wanywao [divai sana, NW]”—hao ndio wale ambao ‘hawana hekima.’
-