Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 6/1 uku. 29
  • Afanywa Mwenye Hekima kwa “Kutozwa Faini”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Afanywa Mwenye Hekima kwa “Kutozwa Faini”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 6/1 uku. 29

Afanywa Mwenye Hekima kwa “Kutozwa Faini”

MITHALI 21:11, NW inasema: “Kwa kutozwa faini kwa mdhihaki asiye na ujuzi hupata hekima; na kwa mmoja kutoa mtazamo wa ndani kwa mtu mwenye hekima yeye hupata maarifa ya kujua.”

Mara nyingi “asiye na ujuzi” ana tatizo la kuthamini kwa nini mwendo fulani wa tendo ni mbaya. Ingawaje, huenda yeye akamwona “mdhihaki”​—mmoja ambaye anadharau kanuni za Neno la Mungu—anashikwa katika uovu wake na kuteseka kwa “dhiki na taabu.” (Mithali 1:27) Chini ya Sheria ya Musa, ‘adhabu’ inayofaa (King James Version), au kwa njia halisi zaidi “faini,” ingetozwa mkosaji.​—Linganisha Kutoka 21:22; Kumbukumbu 22:19.

Tokeo lingekuwa nini kwa mmoja asiye na ujuzi? Kwa kuona thawabu ya kutenda kosa hatimaye, yeye ‘angekuwa mwenye hekima’ na aamue kutofuata mwendo kama huo yeye mwenyewe. (Linganisha Mithali 19:25.) Kwa kutofautiana, “mtu mwenye hekima” tayari anajua kutokana na maono yaliyopita, mambo ambayo amechunguza-chunguza, na maarifa ya kujua kanuni za Biblia kwamba mwenendo fulani wa tendo ni mbaya au wenye kuharibu. Yeye sikuzote hahitaji kuchunguza matokeo ya mwisho yenye kuangamiza ya tendo fulani ili asadikishwe juu ya ubaya walo. Hivyo yeye anaweza kupata ‘mitazamo mipya ya ndani’ kwa agizo tu, badala ya kupatwa na mambo machungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki