Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Baba Mwenye Wana Waasi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 11, 12. (a) Fafanua hali mbaya ya Yuda. (b) Kwa nini hatupaswi kusikitikia Yuda?

      11 Kisha Isaya ajitahidi kusababu na watu wa Yuda kwa kuwatajia hali yao dhaifu. Asema hivi: “Mbona mnataka kupigwa hata sasa, hata mkazidi kuasi?” Kwa maneno mengine Isaya anawauliza: ‘Kwani hamjateseka vya kutosha? Kwa nini mjiletee madhara zaidi kwa kuendelea kuasi?’ Isaya aendelea: “Kichwa chote ni kigonjwa, moyo wote umezimia. Tangu wayo wa mguu hata kichwani hamna uzima ndani yake.” (Isaya 1:5, 6a) Yuda iko katika hali yenye kuchukiza, ya ugonjwa—ugonjwa wa kiroho tangu kichwa hata wayo. Dalili yenye kuhuzunisha kama nini!

      12 Je, tuisikitikie Yuda? Hasha! Karne kadhaa mapema taifa zima la Israeli lilionywa ipasavyo juu ya adhabu ya kutotii. Waliambiwa hivi kwa sehemu: “BWANA atakupiga magoti na miguu kwa jipu lililo zito, usilopata kupozwa, tokea wayo wa mguu mpaka utosi wa kichwa.” (Kumbukumbu la Torati 28:35) Kitamathali, Yuda sasa inapata matokeo hayohayo ya mwenendo wake wa ukaidi. Hayo yote yangeweza kuepukwa iwapo tu watu wa Yuda wangemtii Yehova.

      13, 14. (a) Yuda imepata majeraha gani? (b) Je, mateso ya Yuda huifanya iache mwenendo wake wa uasi?

      13 Isaya aendelea kufafanua hali yenye kusikitisha ya Yuda: “Bali jeraha na machubuko na vidonda vitokavyo usaha; havikufungwa, havikuzongwa-zongwa, wala havikulainishwa kwa mafuta.” (Isaya 1:6b) Hapa nabii huyo arejezea aina tatu ya majeraha: majeraha (kukatwa, kama vile kwa upanga au kisu), machubuko (uvimbe unaosababishwa na pigo), na vidonda (vidonda vya hivi karibuni, vilivyo wazi na vinavyoonekana kuwa haviwezi kupona). Wazo linalotolewa ni la mtu ambaye ameadhibiwa vikali kwa njia zote ziwezekanazo, na mwili wake wote umepata madhara. Hakika Yuda iko katika hali ya kukata tamaa.

      14 Je, hali yenye taabu ya Yuda huifanya imrudie Yehova? La! Yuda ni kama mwasi anayetajwa katika Mithali 29:1: “Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, atavunjika ghafula, wala hapati dawa.” Yaonekana taifa hilo haliwezi kupona. Kama asemavyo Isaya, majeraha yake ‘hayakufungwa, hayakuzongwa-zongwa wala kulainishwa kwa mafuta.’b Kwa njia fulani, Yuda yafanana na kidonda kilicho wazi, kisichofungwa bendeji, na kilichoenea kotekote.

      15. Twaweza kujilindaje dhidi ya ugonjwa wa kiroho?

      15 Twapaswa kujifunza kutokana na Yuda, na tujilinde dhidi ya ugonjwa wa kiroho. Sawa na ugonjwa wa kimwili, ugonjwa huo waweza kudhuru yeyote kati yetu. Kwani, ni nani kati yetu asiyeweza kupatwa na tamaa za kimwili? Pupa na tamaa ya kupata raha kupita kiasi zaweza kusitawi mioyoni mwetu. Basi twahitaji kujizoeza ‘kukirihi lililo ovu’ na ‘kuambatana na lililo jema.’ (Waroma 12:9) Twahitaji pia kukuza matunda ya roho ya Mungu katika maisha yetu ya kila siku. (Wagalatia 5:22, 23) Tukifanya hivyo, tutaepuka janga lililopata Yuda—hali ya kuwa wagonjwa kiroho tangu kichwa mpaka wayo.

  • Baba Mwenye Wana Waasi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • b Maneno ya Isaya yadhihirisha mazoea ya kitiba ya siku yake. Mtafiti wa Biblia E. H. Plumptre ataarifu hivi: “Utaratibu uliojaribiwa kwanza ni ‘kufunga’ au ‘kuminya’ kidonda ili kuondoa usaha; kisha, kama katika kisa cha Hezekia (sura ya 38:21), ‘kilizongwa-zongwa,’ na dawa ya kupaka, kisha mafuta fulani au marhamu yenye kutuliza, labda kama katika Luka 10:34, mafuta na divai vilitumiwa kusafisha kidonda hicho.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki