Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 14. Babiloni ‘atafiwa na watoto na kuwa mjane’ kwa njia zipi?

      14 Ni matokeo gani yatakayompata Babiloni? Yehova anaendelea kusema hivi: “Lakini mambo haya mawili yatakupata katika dakika moja siku moja, kufiwa na watoto, na ujane; yatakupata kiasi kitimilifu, uchawi wako ujapokuwa mwingi, na uganga wako mwingi mno.” (Isaya 47:9) Naam, ukuu wa Babiloni akiwa serikali kubwa ya ulimwengu utakoma ghafula. Katika nchi za kale za Mashariki, kuwa mjane na kufiwa na watoto ndiyo maafa makubwa zaidi ambayo yangeweza kumpata mwanamke. Hatujui Babiloni anafiwa na “watoto” wangapi usiku wa anguko lake.d Ingawa hivyo, wakati utawadia jiji hilo liwe mahame kabisa. (Yeremia 51:29) Pia, ujane utamfika Babiloni kwa kuwa wafalme wake watang’olewa.

      15. Licha ya Babiloni kuwatenda Wayahudi ukatili, ni sababu gani zaidi inayomfanya Yehova amghadhibikie?

      15 Hata hivyo, hasira kali ya Yehova haiji kwa sababu tu ya dhuluma ambazo Babiloni anawatenda Wayahudi. Pia ‘uchawi wake mwingi’ unaichochea hasira ya Yehova. Sheria ya Mungu kwa Israeli hushutumu zoea la kuwasiliana na roho waovu; ingawa hivyo, Babiloni huyafuatia sana mafumbo ya roho. (Kumbukumbu la Torati 18:10-12; Ezekieli 21:21) Kitabu Social Life Among the Assyrians and Babylonians kinasema kwamba Wababiloni waliishi ‘wakiwahofu daima roho wengi sana waovu ambao waliamini kuwa wamewazunguka.’

  • Mwisho Wenye Kutazamisha wa Dini ya Uwongo Waonekana Kimbele
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • d Kitabu Nabonidus and Belshazzar, kilichoandikwa na Raymond Philip Dougherty, kinasema kwamba, ingawa Tarihi za Nabonidus hudai kwamba waliovamia Babiloni waliingia “bila kupigana,” mwanahistoria Mgiriki Xenophon huonyesha kuwa huenda ikawa damu nyingi ilimwagika.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki