Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Msiwatumainie Wakuu”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 9. Shilo ni nani, naye ni mwalimu wa aina gani?

      9 Karne zinapita. “Kikomo kamili cha wakati” kinawasili, kisha yule aitwaye Shilo, yaani Bwana Yesu Kristo, anatokea duniani. (Wagalatia 4:4; Waebrania 1:1, 2) Kwa kuwa Yehova amemteua mwandamani wake wa karibu zaidi kuwa Msemaji wake kwa Wayahudi, hiyo inaonyesha kwamba Yehova anawapenda sana watu wake. Yesu anakuwa msemaji wa aina gani? Wa hali ya juu kabisa! Licha ya Yesu kuwa msemaji, yeye ni mwalimu pia—Mwalimu Stadi. Hiyo haishangazi, kwa maana anafunzwa na Mfunzi wa ajabu—Yehova Mungu mwenyewe. (Yohana 5:30; 6:45; 7:15, 16, 46; 8:26) Jambo hilo linahakikishwa na yale ambayo Yesu anasema kiunabii kupitia Isaya: “Bwana MUNGU amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno [“neno,” “NW”] yeye aliyechoka, huniamsha asubuhi baada ya asubuhi; huniamsha, sikio langu lipate kusikia kama watu wafundishwao.”—Isaya 50:4.b

      10. Yesu anaigaje upendo wa Yehova kwa watu Wake, na anaitikiwa jinsi gani?

      10 Kabla Yesu hajaja duniani, alifanya kazi akiwa karibu na Baba yake mbinguni. Uhusiano mchangamfu ulio kati ya Baba na Mwana unaelezwa kishairi kwenye Mithali 8:30: “Ndipo nilipokuwa pamoja naye [Yehova], kama stadi wa kazi; . . . nikifurahi daima mbele zake.” Yesu alipata shangwe kubwa kwa kumsikiliza Baba yake. Aliwapenda “wanadamu” jinsi Baba yake alivyowapenda. (Mithali 8:31) Yesu anapokuja duniani, anamjibu ‘kwa neno yeye aliyechoka.’ Anaanza huduma yake kwa kusoma kifungu chenye faraja kutoka unabii wa Isaya: “Roho ya Yehova iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kutangaza habari njema kwa walio maskini, . . . kuacha waliopondeka waende zao wakiwa wameachiliwa.” (Luka 4:18; Isaya 61:1) Lo, habari njema kwa maskini! Burudisho kwa waliochoka sana! Tangazo hilo linapaswa kuwaletea watu shangwe iliyoje! Wengine wanashangilia—lakini si wote. Mwishowe, wengi wanazikataa sifa zinazotambulisha kwamba Yesu alifundishwa na Yehova.

      11. Ni nani wanaokuja chini ya nira pamoja na Yesu, nao wanapata nini?

      11 Hata hivyo, wengine wanataka kusikia mengi zaidi. Wanaterema kupata mwaliko huu wa Yesu unaochangamsha moyo: “Njoni kwangu, nyinyi nyote mnaomenyeka na kulemezwa mizigo, nami hakika nitawaburudisha nyinyi. Chukueni nira yangu juu yenu na mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole na wa hali ya chini moyoni, nanyi mtapata burudisho kwa ajili ya nafsi zenu.” (Mathayo 11:28, 29) Kati ya watu wanaomkaribia Yesu, kuna wale wanaume ambao baadaye wanakuwa mitume wake. Wanajua kwamba ili waje wawe na Yesu chini ya nira moja, ni lazima watie bidii. Mojawapo la mambo yanayohusika katika bidii hiyo ni kuzihubiri habari njema za Ufalme hadi miisho ya dunia. (Mathayo 24:14) Mitume na wanafunzi wengine wanapojihusisha na kazi hiyo, wanakuta kwamba kwa kweli inaburudisha nafsi zao. Kazi hiyo hiyo inatimizwa na Wakristo waaminifu leo, nao wanapata shangwe za namna ile ile kwa kuishiriki.

  • “Msiwatumainie Wakuu”
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • b Kuanzia mstari wa 4 hadi mwisho wa sura hiyo, inaonekana mwandishi anaongea kuhusu yeye mwenyewe. Huenda ikawa Isaya alipatwa na baadhi ya majaribu anayoyataja katika mistari hiyo. Lakini, katika maana kamili, unabii huo unatimizwa kuhusiana na Yesu Kristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki