Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Na Tunyoshe Mambo”
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 5. Ni yapi baadhi ya matendo ya ibada wanayoyatenda Wayahudi, na kwa nini hayo ‘yamemlemea’ Yehova?

      5 Si ajabu kwamba sasa Yehova atumia maneno makali! “Msilete tena matoleo ya ubatili; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; siyawezi maovu hayo na makutano ya ibada. Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua.” (Isaya 1:13, 14) Matoleo ya nafaka, uvumba, Sabato, na makutano ya ibada yote hayo ni sehemu ya Sheria ya Mungu kwa Israeli. Kuhusu “mwezi mpya,” Sheria huagiza tu kwamba sikukuu hizo ziadhimishwe, ingawa mapokeo yafaayo yameanzishwa kuhusiana nazo. (Hesabu 10:10; 28:11) Mwezi mchanga huonwa kuwa sabato ya kila mwezi, wakati ambapo watu wangeacha kufanya kazi na hata kukusanyika ili kufundishwa na manabii na makuhani. (2 Wafalme 4:23; Ezekieli 46:3; Amosi 8:5) Hayo si mazoea mabaya. Kasoro ni kwamba yanafanywa ili kujionyesha tu. Isitoshe, Wayahudi wanatenda “maovu,” na kuwasiliana na roho, wakati uleule wakiendelea kushika rasmi Sheria ya Mungu.b Kwa hiyo, ibada yao ‘yamlemea’ Yehova.

  • “Na Tunyoshe Mambo”
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • b Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “maovu” pia latafsiriwa “mambo yanayoumiza,” “yaliyo ya ajabu,” na “mapotovu.” Kwa mujibu wa Theological Dictionary of the Old Testament, manabii Waebrania walilitumia neno hilo kushutumu “uovu uliosababishwa na matumizi mabaya ya mamlaka.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki