Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni Pote
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Nuru Tukufu ya Ukubali wa Mungu

      27. “Mwanamke” wa Yehova huangaziwa nuru gani?

      27 Yehova anaeleza kwamba Yerusalemu ataangaziwa nuru nyingi sana, anaposema hivi: “Jua halitakuwa nuru yako tena wakati wa mchana, wala mwezi hautakupa nuru kwa mwangaza wake; bali BWANA atakuwa nuru ya milele kwako, na Mungu wako atakuwa utukufu wako. Jua lako halitashuka tena, wala mwezi wako hautajitenga; kwa kuwa BWANA mwenyewe atakuwa nuru yako ya milele; na siku za kuomboleza kwako zitakoma.” (Isaya 60:19, 20) Yehova ataendelea kuwa “nuru ya milele” kwa “mwanamke” wake. ‘Hatashuka’ kamwe kama jua la machweo, wala ‘kujitenga’ kama mwezi.d Nuru yake ya kibali cha daima inawaangazia Wakristo watiwa-mafuta, wawakilishi wa kibinadamu wa “mwanamke” wa Mungu. Wao, pamoja na umati mkubwa, wanafurahia nuru kubwa ajabu ya kiroho isiyoweza kuzimwa na giza lolote la kisiasa wala la kiuchumi. Kisha wana hakika ya kuupata wakati ujao mwangavu ambao Yehova ameweka mbele yao.—Waroma 2:7; Ufunuo 21:3-5.

  • Ibada ya Kweli Yapanuka Ulimwenguni Pote
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • d Mtume Yohana anatumia usemi kama huo anapoeleza kuhusu “Yerusalemu jipya,” wale 144,000 wakiwa katika utukufu wa kimbingu. (Ufunuo 3:12; 21:10, 22-26) Hiyo inafaa, kwa maana “Yerusalemu jipya” linawakilisha washirika wote wa Israeli wa Mungu baada ya wao kupokea thawabu yao ya kimbingu, na hivyo kujumlika pamoja na Yesu Kristo kuwa sehemu ya jiji kuu la “mwanamke” wa Mungu, “Yerusalemu la juu.”—Wagalatia 4:26.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki