-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
16. Ni nani wamekuwa wakiwasaidia Wakristo watiwa-mafuta katika kazi yao ya kurudisha ibada safi, na wamekabidhiwa majukumu yapi?
16 Huo ulikuwa utume mkubwa sana. Wale mabaki wa Israeli wa Mungu walio wachache kwa ulinganisho wangetimizaje jukumu hilo? Yehova alimpulizia Isaya kutangaza hivi: “Wageni watasimama na kulisha makundi yenu, na watu wa kabila nyingine watakuwa wakulima wenu, na watunzaji wa mizabibu yenu.” (Isaya 61:5) Kwa njia ya mfano, wageni hao na watu walio wa kabila nyingine wamekuwa “umati mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Yesu.a (Ufunuo 7:9; Yohana 10:11, 16) Wao hawatiwi mafuta kwa roho takatifu kupata urithi wa kimbingu. Bali, wana tumaini la kupata uhai wa milele katika dunia-paradiso. (Ufunuo 21:3, 4) Na bado, wanampenda Yehova na wamekabidhiwa wajibu wa kiroho wa kufanya uchungaji, ukulima, na utunzaji wa mizabibu. Utendaji huo si kazi za hali ya chini. Chini ya mwelekezo wa mabaki wa Israeli wa Mungu, wafanyakazi hawa husaidia kuchunga, kulea, na kuvuna watu.—Luka 10:2; Matendo 20:28; 1 Petro 5:2; Ufunuo 14:15, 16.
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
a Isaya 61:5 yaweza kuwa ilitimizwa nyakati za kale, kwa kuwa watu wasio Wayahudi waliambatana na Wayahudi wa asili wakati wa kurudi kwao Yerusalemu, na inaelekea walisaidia kuirudishia nchi hali yake ya kwanza. (Ezra 2:43-58) Hata hivyo, kuanzia mstari wa 6 unabii unaelekea kutumika kuhusu Israeli wa Mungu peke yake.
-