-
Yehova Ajifanyia Jina MaridadiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
19, 20. Wayahudi wanakumbuka mambo gani, na kwa nini?
19 Katikati ya mateso yao, Wayahudi fulani wanaguswa moyo kuufikiria wakati uliopita. Isaya anasema hivi: “Ndipo walipokumbuka siku za zamani, wakati wa Mose mtumishi wa Mwenyezi-Mungu. Wakauliza, ‘Yuko wapi sasa Mwenyezi-Mungu, aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake baharini? Yuko wapi yule aliyeiweka roho yake takatifu kati yao, ambaye kwa mkono wake wenye nguvu [“maridadi,” “NW”] alifanya maajabu kwa njia ya Mose, akapasua bahari na kuwaongoza watu wake, na kujipatia jina la milele? Aliwaongoza katikati ya vilindi vya bahari, wakapita humo kama farasi bila kujikwaa. Kama ng’ombe wapelekwavyo malishoni bondeni, ndivyo roho ya Mungu ilivyowapumzisha watu wake.”—Isaya 63:11-14a, “BHN.”d
20 Ndiyo, kwa kupatwa na matokeo ya kutokutii, Wayahudi wanatamani sana siku zile ambazo Yehova alikuwa Mkombozi wao wala si adui yao. Wanakumbuka jinsi “wachungaji” wao, Musa na Haruni, walivyowaongoza salama wakawavusha Bahari Nyekundu. (Zaburi 77:20; Isaya 51:10) Wanakumbuka wakati ambao, badala ya wao kuihuzunisha roho ya Mungu, roho hiyo iliwaongoza kupitia mwelekezo uliotolewa na Musa na wanaume wengine wazee waliowekwa rasmi kwa roho. (Hesabu 11:16, 17) Vilevile wanakumbuka ya kwamba waliona ‘mkono maridadi’ wa nguvu za Yehova ukitumiwa kwa niaba yao kupitia Musa! Baada ya muda, Mungu aliwaondoa katika lile jangwa kubwa la kuogofya, akawaongoza kuwaingiza nchi inayotiririka maziwa na asali—mahali pa pumziko. (Kumbukumbu la Torati 1:19; Yoshua 5:6; 22:4) Ingawa hivyo, sasa Waisraeli wanateseka kwa sababu wamepoteza uhusiano wao mzuri na Mungu!
-
-
Yehova Ajifanyia Jina MaridadiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
d Mstari huu ungeweza pia kuanza kwa kusema hivi: “Yeye akaanza kukumbuka.” (Isaya 63:11, kielezi-chini katika NW) Hata hivyo, si lazima hiyo imaanishe kwamba Yehova ndiye mwenye kukumbuka. Maneno yanayofuata yanaeleza hisia za watu wa Mungu wala si za Yehova mwenyewe. Hivyo, kichapo Soncino Books of the Bible kinayafasiri maneno hayo hivi: “Ndipo watu Wake wakazikumbuka siku za zamani.”
-