-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
18. Wale ambao wamemwacha Yehova watabaki na kitu gani, na kuapa kwa jina lao huenda kukawa kunadokeza nini?
18 Yehova anaendelea kuongea na wale ambao wamemwacha: “Nanyi mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa wateule wangu. Na Bwana MUNGU atakuua; naye atawaita watumishi wake kwa jina lingine. Hata itakuwa yeye atakayejibariki duniani, atajibariki kwa Mungu wa kweli; naye atakayeapa duniani, ataapa kwa Mungu wa kweli. Kwa kuwa taabu za kwanza zimesahauliwa, na kwa kuwa zimefichwa machoni pangu.” (Isaya 65:15, 16) Wale ambao wamemwacha Yehova watabaki na jina lao tu, nalo litatumika katika kuapa tu, au kulaani. Huenda hiyo ikamaanisha kwamba wale wanaotaka kujifunga kwa kiapo kizito, watakuwa ni kama wanasema hivi: ‘Nisipotimiza ahadi hii, acha nipatwe na adhabu iliyowapata wale waasi-imani.’ Huenda hata ikamaanisha kwamba jina lao litatumiwa kwa njia ya mfano, kama Sodoma na Gomora, ili liwe mfano wa adhabu ya Mungu juu ya waovu.
19. Watumishi wa Mungu wataitwaje jina jingine, na kwa nini watakuwa na uhakika wa kumwamini yule Mungu wa uaminifu? (Ona pia kielezi-chini.)
19 Lakini hali ya watumishi wa Mungu itakuwa tofauti kama nini! Wataitwa jina jingine. Hiyo ni kuonyesha kwamba watabarikiwa na kuheshimiwa wakiisha kurudi katika nchi ya kwao. Hawatatafuta baraka kwa mungu yeyote wa uwongo wala hawataapa kwa jina la sanamu yoyote isiyo na uhai. Bali, wanapojibariki au kuapa, watafanya hivyo kwa jina la yule Mungu wa uaminifu. (Isaya 65:16, kielezi-chini katika tafsiri ya NW) Wakaaji wa nchi watakuwa na sababu ya kumwamini Mungu wakiwa na uhakika kabisa, kwani atakuwa amethibitisha kuwa yeye ni mtimizaji wa ahadi zake.c Wayahudi wakiisha kuwa salama nchini mwao, wataisahau upesi misononeko iliyowapata zamani.
-
-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
c Kulingana na Isaya 65:16 katika maandishi ya Kimasoreti ya Kiebrania, Yehova ndiye “Mungu wa Ameni.” “Ameni” humaanisha “na iwe hivyo,” au “ni hakika,” na hilo ni neno la kutoa uthibitisho au uhakikisho wa kwamba jambo fulani ni la kweli au ni sharti litimie. Kwa kutimiza ahadi zake zote, Yehova anaonyesha kwamba yale anayoyasema ni ya kweli.
-