Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 29. (a) Watu wa Mungu walio watiifu watapata shangwe zipi katika nchi ya Yuda iliyorudishwa? (b) Kwa nini miti ni mfano unaofaa wa maisha marefu? (Ona kielezi-chini.)

      29 Yehova anaendelea kueleza juu ya hali zitakazokuwako katika nchi iliyorudishwa ya Yuda: “Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.” (Isaya 65:21, 22) Baada ya kuirudia nchi ya Yuda, ambayo bila shaka haikuwa na nyumba wala mizabibu, watu wa Mungu walio watiifu watakuwa na shangwe ya kuishi katika nyumba zao wenyewe na kula matunda kutoka mashamba yao wenyewe ya mizabibu. Mungu ataibariki kazi yao, na wataishi maisha marefu—marefu kama siku za mti—wafurahie matunda ya kazi zao.e

      30. Watumishi wa Yehova wanafurahia hali gani leo, na watafurahia nini katika ulimwengu mpya?

      30 Unabii huu umepata utimizo fulani katika siku zetu. Watu wa Yehova walitoka kwenye uhamisho wa kiroho mwaka wa 1919, wakaanza kurudisha hali za kwanza katika “nchi” au makao yao ya utendaji na ibada. Walijenga makutaniko na kusitawisha hali ya kuzaa matunda ya kiroho. Matokeo ni kwamba, hata sasa watu wa Yehova wanafurahia paradiso ya kiroho na amani waliyopewa na Mungu. Tunaweza kuwa na hakika kwamba amani hiyo itaendelea mpaka ndani ya ile Paradiso halisi. Hata haiwezekani kuwaza kwa usahihi ni maajabu gani ambayo Yehova atafanya katika ulimwengu mpya kwa kuitumia mioyo na mikono ya waabudu wake wenye nia ya kufanya kazi. Itakuwa shangwe iliyoje kujenga nyumba yako mwenyewe kisha kuishi ndani yake! Chini ya utawala wa Ufalme, hakutakuwako upungufu wa kazi ya kuridhisha. Utafurahi kama nini “kujiburudisha kwa mema” ya matunda ya kazi zako mwenyewe sikuzote! (Mhubiri 3:13) Je, tutapata wakati wa kutosha kuifurahia sana kazi ya mikono yetu? Kabisa! Maisha yasiyo na kikomo ya wanadamu waaminifu yatakuwa “kama siku za mti”—maelfu ya miaka, na hata zaidi!

  • ‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • e Miti ni mfano unaofaa wa maisha marefu kwa maana ina maisha marefu kuliko vitu vingine vyote vilivyo hai vinavyojulikana. Kwa mfano, mzeituni huzaa matunda kwa mamia ya miaka, na huenda ukaishi hata miaka elfu moja.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki