Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Tafadhali, Itii Sauti ya Yehova”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • 12. Wakati mwingine wazee hulazimika kufanya nini ili kulinda kutaniko?

      12 Wayahudi wengi walidharau msaada ambao Yehova aliwapa tena na tena kupitia Yeremia. Vivyo hivyo, huenda mtu ambaye amefanya dhambi nzito leo akakataa kutubu, na kukataa msaada wa wazee. Katika hali hiyo, wazee watafuata mwongozo wa Kimaandiko wa kulinda kutaniko kwa kumtenga na ushirika mkosaji huyo. (1 Kor. 5:11-13; ona sanduku “Kuishi Bila Sheria,” katika ukurasa wa 73.) Hata hivyo, je, hilo linamaanisha kwamba huo ndio mwisho wa mambo, kwamba mtu huyo hawezi kamwe kumrudia Yehova? Hapana. Ingawa Waisraeli waliasi kwa muda mrefu, bado Mungu aliwaambia: “Rudini, ninyi wana waasi. Nitaiponya hali yenu ya uasi.” (Yer. 3:22)a Yehova anawaalika wakosaji wamrudie. Na si kuwaalika tu, bali anawaagiza wafanye hivyo.

      KUISHI BILA SHERIA

      Wayahudi waliishi maisha ya aina gani baada ya Yerusalemu kuharibiwa? Yeremia anatueleza kifupi kwenye Maombolezo 2:9. Kuta za Yerusalemu zilikuwa zimebomolewa, huenda hata malango ya jiji hilo. Isitoshe, ‘hawakuwa na sheria.’ Je, Yeremia alimaanisha kwamba watu waliookoka uharibifu huo walikuwa umati wenye fujo? Yaelekea alimaanisha kwamba wamepoteza ulinzi wa kiroho na hali nzuri waliyokuwa wakifurahia wakati ambapo makuhani waaminifu na manabii walikuwa wakiwafundisha Sheria ya Mungu. Sasa manabii wa uwongo waliowategemea hawakuwa na ‘maono’ ya kweli, au mwongozo, kutoka kwa Yehova; “maono” yao yalikuwa ya ubatili.—Omb. 2:14.

      Huenda mtu ambaye ametengwa na ushirika wa kutaniko la Kikristo akajiona hivyo. Anakosa ushirika wenye upendo wa ndugu na dada zake wa kiroho na wazee wanaomjali. Amepoteza mwongozo wa kiroho. Katika ulimwengu ‘usio na sheria’ kutoka kwa Yehova, huenda anahisi kuwa amepata hasara kubwa. Vyovyote vile, anaweza kurudi na kupata kibali cha Yehova na kufurahia baraka nyingi tena. (2 Kor. 2:6-10) Hata hivyo, kumtii Yehova na kuendelea kuishi kupatana na sheria ni bora kuliko kuishi bila sheria.

  • “Tafadhali, Itii Sauti ya Yehova”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
    • a Yehova alikuwa akizungumza na taifa la kaskazini la Israeli. Watu wa ufalme huo wa makabila kumi walikuwa uhamishoni kwa miaka 100 hivi Yeremia alipotangaza ujumbe huo. Alikiri kwamba hata kufikia siku zake, bado taifa hilo halikuwa limetubu. (2 Fal. 17:16-18, 24, 34, 35) Hata hivyo, watu mmoja-mmoja wangeweza kupata tena kibali cha Mungu, na hata kurudi kutoka uhamishoni.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki