-
“Tafadhali, Itii Sauti ya Yehova”Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
12. Wakati mwingine wazee hulazimika kufanya nini ili kulinda kutaniko?
12 Wayahudi wengi walidharau msaada ambao Yehova aliwapa tena na tena kupitia Yeremia. Vivyo hivyo, huenda mtu ambaye amefanya dhambi nzito leo akakataa kutubu, na kukataa msaada wa wazee. Katika hali hiyo, wazee watafuata mwongozo wa Kimaandiko wa kulinda kutaniko kwa kumtenga na ushirika mkosaji huyo. (1 Kor. 5:11-13; ona sanduku “Kuishi Bila Sheria,” katika ukurasa wa 73.) Hata hivyo, je, hilo linamaanisha kwamba huo ndio mwisho wa mambo, kwamba mtu huyo hawezi kamwe kumrudia Yehova? Hapana. Ingawa Waisraeli waliasi kwa muda mrefu, bado Mungu aliwaambia: “Rudini, ninyi wana waasi. Nitaiponya hali yenu ya uasi.” (Yer. 3:22)a Yehova anawaalika wakosaji wamrudie. Na si kuwaalika tu, bali anawaagiza wafanye hivyo.
-
-
“Tafadhali, Itii Sauti ya Yehova”Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
-
-
a Yehova alikuwa akizungumza na taifa la kaskazini la Israeli. Watu wa ufalme huo wa makabila kumi walikuwa uhamishoni kwa miaka 100 hivi Yeremia alipotangaza ujumbe huo. Alikiri kwamba hata kufikia siku zake, bado taifa hilo halikuwa limetubu. (2 Fal. 17:16-18, 24, 34, 35) Hata hivyo, watu mmoja-mmoja wangeweza kupata tena kibali cha Mungu, na hata kurudi kutoka uhamishoni.
-