-
Je, Una ‘Moyo Wa Kumjua’ Yehova?Mnara wa Mlinzi—2013 | Machi 15
-
-
8, 9. Wayahudi wengi walihitaji kufanya nini kuhusu moyo wao?
8 Tunapata dokezo kuhusu maana ya usemi ‘wasiotahiriwa moyoni’ tunapochunguza jambo ambalo Mungu aliwahimiza Wayahudi wafanye: ‘Ondoeni magovi ya mioyo yenu, ninyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu; ili ghadhabu yangu isitoke kwa sababu ya ubaya wa matendo yenu.’ Lakini matendo yao mabaya yalitoka wapi? Yalitoka ndani ya moyo wao. (Soma Marko 7:20-23.) Naam, kupitia Yeremia, Mungu alieleza kwa usahihi chanzo cha matendo mabaya ya Wayahudi hao. Moyo wao ulikuwa mgumu na wenye kuasi. Nia na mawazo yao hayakumpendeza. (Soma Yeremia 5:23, 24; 7:24-26.) Mungu aliwaambia hivi: “Tahiriweni kwa ajili ya Yehova, na kuondoa magovi ya mioyo yenu.”—Yer. 4:4; 18:11, 12.
9 Hivyo, Wayahudi katika siku za Yeremia walihitaji upasuaji wa moyo wa mfano, yaani, ‘kutahiriwa moyoni,’ sawa na Waisraeli katika siku za Musa. (Kum. 10:16; 30:6) ‘Kuondoa magovi ya mioyo yao’ kulimaanisha kuondolea mbali mambo yaliyofanya mioyo yao iwe migumu, yaani, mawazo yao, nia, au mapendezi yaliyopingana na ya Mungu.—Mdo. 7:51.
-
-
Je, Una ‘Moyo Wa Kumjua’ Yehova?Mnara wa Mlinzi—2013 | Machi 15
-
-
11, 12. (a) Kwa nini kila mmoja wetu anapaswa kuuchunguza moyo wake mwenyewe? (b) Mungu hatafanya nini?
11 Yehova anataka kila mmoja wetu asitawishe na kudumisha hali inayokubalika machoni pake. Yeremia alikiri hivi kuhusu mtu mwadilifu: “Wewe, Ee Yehova wa majeshi, unamchunguza mwadilifu; unaziona figo na moyo.” (Yer. 20:12) Ikiwa Mweza-Yote anauchunguza hata moyo wa mtu mwadilifu, je, hatupaswi kujichunguza wenyewe kwa unyoofu? (Soma Zaburi 11:5.) Tunapofanya hivyo, huenda tukagundua mtazamo, lengo, au hisia fulani ya ndani tunayohitaji kurekebisha. Tunaweza kutambua jambo fulani linalofanya moyo wetu uwe mgumu au huenda ‘moyo wetu una govi’ la mfano linalopasa kuondolewa. Huo ndio upasuaji wa moyo wa mfano. Ikiwa unakubali kwamba ni vizuri uuchunguze moyo wako wa mfano, utafute nini? Na unawezaje kufanya marekebisho yoyote yanayohitajiwa?—Yer. 4:4.
-