Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mtakuwa Hai”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 12 Baadaye, Charles T. Russell na washiriki wake walijitahidi kurudisha kweli za Biblia, ni kana kwamba “kano na nyama” ziliungana na mifupa. Gazeti la Zion’s Watch Tower na machapisho mengine yaliwasaidia watu wenye mioyo minyoofu watambue kweli za Biblia, ambazo ziliwachochea kujiunga na watumishi wa Mungu waliotiwa mafuta. Mwanzoni mwa miaka ya 1900, watumishi wa Mungu waliotiwa mafuta walizidi kutiwa nguvu na vifaa kama vile “Photo-Drama of Creation” na kitabu The Finished Mystery. Baada ya muda mfupi, wakati wa Mungu kufanya watu wake ‘wasimame kwa miguu yao’ ukafika. (Eze. 37:10) Jambo hilo lilitukia lini na jinsi gani? Matukio yaliyotukia katika Babiloni la kale yanatusaidia kujibu swali hilo.

      “Wakaanza Kuishi na Kusimama kwa Miguu Yao”

      13. (a) Kuanzia mwaka wa 537 K.W.K., maneno ya Ezekiel 37:10, 14 yalitimizwaje? (b) Ni maandiko gani yanayoonyesha kwamba baadhi ya watu kutoka ufalme wa makabila kumi walirudi Israeli?

      13 Kuanzia mwaka wa 537 K.W.K, Wayahudi waliokuwa Babiloni waliona utimizo wa maono hayo. Jinsi gani? Yehova aliwafanya wawe hai na kufanya ‘wasimame kwa miguu yao’ kwa kuwakomboa kutoka katika utekwa na kuwaruhusu warudi Israeli. Kikundi cha Waisraeli 42,360 na watu 7,000 wasio Waisraeli waliondoka Babiloni kwenda kujenga upya Yerusalemu na hekalu lake, na kuishi katika nchi ya Israeli. (Ezra 1:1-4; 2:64, 65; Eze. 37:14) Kisha, miaka 70 hivi baadaye, karibu wahamishwa 1,750 walijiunga na Ezra kurudi Yerusalemu. (Ezra 8:1-20) Basi, kwa ujumla, zaidi ya Wayahudi 44,000 walirudi—kwa kweli lilikuwa “jeshi kubwa.” (Eze. 37:10) Isitoshe, Neno la Mungu linaonyesha kwamba watu wa kutoka ufalme wenye makabila kumi, ambao babu zao walikuwa wamepelekwa utekwani na Waashuru katika karne ya nane K.W.K., pia walirudi Israeli ili kusaidia kujenga upya hekalu.—1 Nya. 9:3; Ezra 6:17; Yer. 33:7; Eze. 36:10.

      Kikundi cha Wakristo watiwa mafuta kuanzia karne ya pili W.K. hadi mwaka wa 1919 W.K.

      SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10B: Kuna Uhusiano Gani Kati ya​—“Mifupa Mikavu” na ‘Mashahidi Wawili’?

      14. (a) Maneno ya Ezekieli 37:24 yanatusaidiaje kutambua wakati wa utimizo mkuu wa unabii huo? (b) Ni jambo gani lililotukia mwaka wa 1919? (Tazama pia sanduku “Kuna Uhusiano Gani Kati ya ‘Mifupa Mikavu’ na “Mashahidi Wawili””)

      14 Sehemu hii ya unabii wa Ezekieli ilitimizwaje kwa njia kubwa zaidi? Kama Yehova alivyomfunulia Ezekieli katika unabii unaohusiana na huu, sehemu kuu ya utimizo wa unabii huu wa kurudishwa ingetimizwa muda fulani baada ya Daudi Mkuu, Yesu Kristo, kuanza kutawala akiwa Mfalme.b (Eze. 37:24) Na kwa kweli, mwaka wa 1919, Yehova aliweka roho yake ndani ya watu wake. Matokeo ni kwamba wakawa “hai” na wakawekwa huru kutoka kwa utekwa wa Babiloni Mkubwa. (Isa. 66:8) Baada ya hapo, Yehova aliwaruhusu waishi katika “nchi” yao, yaani, paradiso ya kiroho. Hata hivyo, watumishi wa siku hizi wa Yehova wamekuwaje “jeshi kubwa”?

      Ndugu mwenye umri mkubwa akitafakari mambo aliyotoka kusoma katika kitabu cha Ezekieli.

      SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10C: Msaada wa Kusimama Tena

      15, 16. (a) Leo, watu wa Yehova wamekuwaje “jeshi kubwa”? (b) Unabii huu wa Ezekieli unatusaidiaje kukabiliana na hali ngumu maishani? (Tazama sanduku “Msaada wa Kusimama Tena.”)

      15 Muda mfupi baada ya Kristo kumweka rasmi mtumwa mwaminifu mwaka wa 1919, watumishi wa Mungu walianza kupatwa na jambo ambalo Zekaria, nabii wa Mungu aliyetumikia kati ya wahamishwa, alikuwa ametabiri aliposema: “Mataifa mengi na mataifa yenye nguvu yatakuja . . . kumtafuta Yehova.” Nabii huyo aliwalinganisha watu hao wanaomtafuta Yehova na “watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa.” Watu hao wangeshika kwa nguvu mavazi ya “Myahudi,” Israeli wa kiroho wakisema: “Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yupo pamoja nanyi.”—Zek. 8:20-23.

      16 Leo, Israeli wa kiroho (watiwa mafuta waliobaki) na vilevile “wanaume kumi” (kondoo wengine) kwa pamoja wanafanyiza “jeshi kubwa ajabu,” lenye mamilioni ya watu. (Eze. 37:10) Tukiwa wanajeshi wa Kristo katika jeshi hilo linalozidi kuongezeka, tunamfuata kwa ukaribu Mfalme wetu Yesu, tukielekea kwenye baraka zilizo mbele yetu.—Zab. 37:29; Eze. 37:24; Flp. 2:25; 1 The. 4:16, 17.

  • Ibada Safi​—Yarudishwa Hatua kwa Hatua
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
      • Nathan H. Knorr, Joseph F. Rutherford, na Hayden C. Covington.

        “Wakaanza kuishi na kusimama kwa miguu yao”

        Baada ya watu wa Yehova kuwa “hai” mwaka wa 1919, waliongeza bidii katika kazi ya kuhubiri

  • “Mtakuwa Hai”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 12 Baadaye, Charles T. Russell na washiriki wake walijitahidi kurudisha kweli za Biblia, ni kana kwamba “kano na nyama” ziliungana na mifupa. Gazeti la Zion’s Watch Tower na machapisho mengine yaliwasaidia watu wenye mioyo minyoofu watambue kweli za Biblia, ambazo ziliwachochea kujiunga na watumishi wa Mungu waliotiwa mafuta. Mwanzoni mwa miaka ya 1900, watumishi wa Mungu waliotiwa mafuta walizidi kutiwa nguvu na vifaa kama vile “Photo-Drama of Creation” na kitabu The Finished Mystery. Baada ya muda mfupi, wakati wa Mungu kufanya watu wake ‘wasimame kwa miguu yao’ ukafika. (Eze. 37:10) Jambo hilo lilitukia lini na jinsi gani? Matukio yaliyotukia katika Babiloni la kale yanatusaidia kujibu swali hilo.

      “Wakaanza Kuishi na Kusimama kwa Miguu Yao”

      13. (a) Kuanzia mwaka wa 537 K.W.K., maneno ya Ezekiel 37:10, 14 yalitimizwaje? (b) Ni maandiko gani yanayoonyesha kwamba baadhi ya watu kutoka ufalme wa makabila kumi walirudi Israeli?

      13 Kuanzia mwaka wa 537 K.W.K, Wayahudi waliokuwa Babiloni waliona utimizo wa maono hayo. Jinsi gani? Yehova aliwafanya wawe hai na kufanya ‘wasimame kwa miguu yao’ kwa kuwakomboa kutoka katika utekwa na kuwaruhusu warudi Israeli. Kikundi cha Waisraeli 42,360 na watu 7,000 wasio Waisraeli waliondoka Babiloni kwenda kujenga upya Yerusalemu na hekalu lake, na kuishi katika nchi ya Israeli. (Ezra 1:1-4; 2:64, 65; Eze. 37:14) Kisha, miaka 70 hivi baadaye, karibu wahamishwa 1,750 walijiunga na Ezra kurudi Yerusalemu. (Ezra 8:1-20) Basi, kwa ujumla, zaidi ya Wayahudi 44,000 walirudi—kwa kweli lilikuwa “jeshi kubwa.” (Eze. 37:10) Isitoshe, Neno la Mungu linaonyesha kwamba watu wa kutoka ufalme wenye makabila kumi, ambao babu zao walikuwa wamepelekwa utekwani na Waashuru katika karne ya nane K.W.K., pia walirudi Israeli ili kusaidia kujenga upya hekalu.—1 Nya. 9:3; Ezra 6:17; Yer. 33:7; Eze. 36:10.

      Kikundi cha Wakristo watiwa mafuta kuanzia karne ya pili W.K. hadi mwaka wa 1919 W.K.

      SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10B: Kuna Uhusiano Gani Kati ya​—“Mifupa Mikavu” na ‘Mashahidi Wawili’?

      14. (a) Maneno ya Ezekieli 37:24 yanatusaidiaje kutambua wakati wa utimizo mkuu wa unabii huo? (b) Ni jambo gani lililotukia mwaka wa 1919? (Tazama pia sanduku “Kuna Uhusiano Gani Kati ya ‘Mifupa Mikavu’ na “Mashahidi Wawili””)

      14 Sehemu hii ya unabii wa Ezekieli ilitimizwaje kwa njia kubwa zaidi? Kama Yehova alivyomfunulia Ezekieli katika unabii unaohusiana na huu, sehemu kuu ya utimizo wa unabii huu wa kurudishwa ingetimizwa muda fulani baada ya Daudi Mkuu, Yesu Kristo, kuanza kutawala akiwa Mfalme.b (Eze. 37:24) Na kwa kweli, mwaka wa 1919, Yehova aliweka roho yake ndani ya watu wake. Matokeo ni kwamba wakawa “hai” na wakawekwa huru kutoka kwa utekwa wa Babiloni Mkubwa. (Isa. 66:8) Baada ya hapo, Yehova aliwaruhusu waishi katika “nchi” yao, yaani, paradiso ya kiroho. Hata hivyo, watumishi wa siku hizi wa Yehova wamekuwaje “jeshi kubwa”?

      Ndugu mwenye umri mkubwa akitafakari mambo aliyotoka kusoma katika kitabu cha Ezekieli.

      SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10C: Msaada wa Kusimama Tena

      15, 16. (a) Leo, watu wa Yehova wamekuwaje “jeshi kubwa”? (b) Unabii huu wa Ezekieli unatusaidiaje kukabiliana na hali ngumu maishani? (Tazama sanduku “Msaada wa Kusimama Tena.”)

      15 Muda mfupi baada ya Kristo kumweka rasmi mtumwa mwaminifu mwaka wa 1919, watumishi wa Mungu walianza kupatwa na jambo ambalo Zekaria, nabii wa Mungu aliyetumikia kati ya wahamishwa, alikuwa ametabiri aliposema: “Mataifa mengi na mataifa yenye nguvu yatakuja . . . kumtafuta Yehova.” Nabii huyo aliwalinganisha watu hao wanaomtafuta Yehova na “watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa.” Watu hao wangeshika kwa nguvu mavazi ya “Myahudi,” Israeli wa kiroho wakisema: “Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yupo pamoja nanyi.”—Zek. 8:20-23.

      16 Leo, Israeli wa kiroho (watiwa mafuta waliobaki) na vilevile “wanaume kumi” (kondoo wengine) kwa pamoja wanafanyiza “jeshi kubwa ajabu,” lenye mamilioni ya watu. (Eze. 37:10) Tukiwa wanajeshi wa Kristo katika jeshi hilo linalozidi kuongezeka, tunamfuata kwa ukaribu Mfalme wetu Yesu, tukielekea kwenye baraka zilizo mbele yetu.—Zab. 37:29; Eze. 37:24; Flp. 2:25; 1 The. 4:16, 17.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki