Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mtakuwa Hai”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • “Mifupa Yetu Imekauka, Nalo Tumaini Letu Limepotea”

      6. Ni maneno gani ya Yehova yaliyomsaidia Ezekieli kuelewa maono hayo?

      6 Kisha Yehova akamfunulia Ezekieli maana ya maono hayo, akisema: “Mifupa hii ni watu wote wa nyumba ya Israeli.” Kwa kweli, baada ya wahamishwa kusikia Yerusalemu limeharibiwa, walihisi kana kwamba wamekufa. Kwa hiyo, wakaomboleza hivi: “Mifupa yetu imekauka, nalo tumaini letu limepotea. Tumeangamizwa kabisa.” (Eze. 37:11; Yer. 34:20) Kisha akijibu maombolezo yao, Yehova alifunua kwamba maono hayo ya mifupa kwa kweli yalikuwa na ujumbe wenye kupendeza wa tumaini kwa Israeli.

  • “Mtakuwa Hai”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 8. (a) “Watu wote wa nyumba ya Israeli” walikuwa katika hali gani inayofanana na kifo? (b) Andiko la Ezekieli 37:9 linaonyeshaje sababu ya kifo cha mfano cha Israeli? (Tazama maelezo ya chini.)

      8 Taifa la kale la Israeli lilikuwa limeonaje utimizo wa sehemu yenye kuhuzunisha ya maono hayo ya kinabii? Kwa njia ya mfano, tayari taifa la Israeli lilikuwa limeanza kufa mwaka wa 740 K.W.K. wakati ufalme wenye makabila kumi ulipoanguka na kupelekwa uhamishoni. Miaka 130 hivi baadaye, watu wa Yuda pia walipopelekwa uhamishoni, “watu wote wa nyumba ya Israeli” wakaenda utekwani. (Eze. 37:11) Kwa njia ya mfano, kikundi chote cha wahamishwa kilikuwa kimekufa kama mifupa ambayo Ezekieli aliona katika maono.a Pia, kumbuka kwamba Ezekieli hakuona tu mifupa bali mifupa “mikavu sana,” jambo lililoonyesha kwamba walikuwa wamekufa kwa muda mrefu sana. Kwa kweli, kwa ujumla Israeli na Yuda walikaa utekwani zaidi ya miaka 200, kuanzia 740 hadi 537 K.W.K.—Yer. 50:33.

  • “Mtakuwa Hai”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • a Mifupa ambayo Ezekieli aliona katika maono, haikuwa ya watu waliokufa kifo cha kawaida, bali ya “watu waliouawa.” (Eze. 37:9) “Watu wote wa nyumba ya Israeli” waliuawa kwa njia ya mfano wakati wakaaji wa ufalme wa Israeli wenye makabila kumi na wale wa ufalme wa Yuda wenye makabila mawili waliposhindwa, wakatekwa, na kupelekwa uhamishoni na Waashuru na Wababiloni.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki