-
Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” YetuMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
13. Ni ponyo gani limetimizwa wakati wetu?
13 Mto huo wa kimaono unaingia katika Bahari ya Chumvi isiyo na uhai na kuponya chochote ambacho hukifikia. Bahari hiyo hufananisha mazingira yaliyokufa kiroho. Lakini uhai watokea kwa wingi ‘kila mahali ufikapo mto huo.’ (Ezekieli 47:9) Vivyo hivyo, katika siku za mwisho, watu wamefanywa hai kiroho kokote ambako maji ya uhai yamepenyeza. Watu wa kwanza kutiwa uhai mpya jinsi hiyo ni baki la watiwa-mafuta mwaka wa 1919. Walirudishwa kighafula kwenye uhai wa kiroho kutoka hali iliyo kama kifo, ya kutotenda. (Ezekieli 37:1-14; Ufunuo 11:3, 7-12) Tangu wakati huo maji hayo ya uhai yamewafikia watu wengine walio wafu kiroho, nao wamekuwa hai na kufanyiza umati mkubwa wa kondoo wengine unaozidi kuongezeka daima, wanaompenda na kumtumikia Yehova. Hivi karibuni, uandalizi huu utafikia halaiki ya watu watakaofufuliwa.
-
-
Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” YetuMnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
18 Wakati wa Milenia, magonjwa yote—ya kimwili, ya kiakili, na ya kihisia-moyo—yataponywa. Hilo laonyeshwa vyema kwa ‘kuponywa kwa mataifa’ kupitia miti hiyo ya ufananisho. Kwa sababu ya maandalizi yatakayotolewa na Kristo pamoja na wale 144,000, “hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isaya 33:24) Nao mto huo utaingia kipindi cha mpanuko wake ulio mkubwa zaidi. Utalazimika kupanuka na kuongezeka kina ili kuwatosheleza mamilioni, labda mabilioni, ya wanadamu waliofufuliwa ambao watayanywa maji hayo safi ya uhai. Mto wa kimaono uliponya Bahari ya Chumvi, ukitokeza uhai popote maji yake yalipotiririka kuelekea. Katika Paradiso, wanaume na wanawake watakuja kwenye uhai kwa maana iliyo kamili zaidi, wakiponywa kutokana na kifo cha Kiadamu kilichorithiwa ikiwa watajizoeza imani katika manufaa za fidia watakazopewa. Ufunuo 20:12 hutabiri kwamba “hati-kunjo” zitafunguliwa katika siku hizo, zikiandaa nuru zaidi ya uelewevu ambao utawanufaisha wale watakaofufuliwa. Kwa kuhuzunisha, hata katika Paradiso, watu fulani watakataa kuponywa. Waasi hao ndio wale ‘walioachiwa chumvi’ ya uharibifu wa milele.—Ufunuo 20:15.
-