Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” Yetu
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
    • 15. Ni nini kionyeshacho kwamba si kila mtu atakayekubali maandalizi ya Mungu ya uhai, nalo tokeo la mwisho ni nini kwa watu kama hao?

      15 Bila shaka, si wote huitikia ujumbe wa uhai ifaavyo sasa; wala si wote watakaofufuliwa wakati wa Utawala wa Milenia wa Kristo wataitikia ifaavyo. (Isaya 65:20; Ufunuo 21:8) Malaika atangaza kwamba sehemu fulani za bahari haziponywi. Sehemu hizo zenye matope, zisizo na uhai ‘zaachwa ziwe za chumvi.’ (Ezekieli 47:11) Kwa habari ya watu wa siku yetu, si wote huyakubali maji ya Yehova yenye kutokeza uhai wanayopewa. (Isaya 6:10) Kwenye Har–Magedoni, wale wote ambao wamechagua kubaki katika hali isiyo na uhai na yenye ugonjwa kiroho wataachiwa chumvi, yaani, wataharibiwa milele. (Ufunuo 19:11-21) Hata hivyo, wale ambao wamekuwa wakinywa maji hayo kwa uaminifu wanaweza kutumaini kuokoka na kuona utimizo wa mwisho wa unabii huu.

  • Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” Yetu
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
    • 18 Wakati wa Milenia, magonjwa yote—ya kimwili, ya kiakili, na ya kihisia-moyo—yataponywa. Hilo laonyeshwa vyema kwa ‘kuponywa kwa mataifa’ kupitia miti hiyo ya ufananisho. Kwa sababu ya maandalizi yatakayotolewa na Kristo pamoja na wale 144,000, “hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isaya 33:24) Nao mto huo utaingia kipindi cha mpanuko wake ulio mkubwa zaidi. Utalazimika kupanuka na kuongezeka kina ili kuwatosheleza mamilioni, labda mabilioni, ya wanadamu waliofufuliwa ambao watayanywa maji hayo safi ya uhai. Mto wa kimaono uliponya Bahari ya Chumvi, ukitokeza uhai popote maji yake yalipotiririka kuelekea. Katika Paradiso, wanaume na wanawake watakuja kwenye uhai kwa maana iliyo kamili zaidi, wakiponywa kutokana na kifo cha Kiadamu kilichorithiwa ikiwa watajizoeza imani katika manufaa za fidia watakazopewa. Ufunuo 20:12 hutabiri kwamba “hati-kunjo” zitafunguliwa katika siku hizo, zikiandaa nuru zaidi ya uelewevu ambao utawanufaisha wale watakaofufuliwa. Kwa kuhuzunisha, hata katika Paradiso, watu fulani watakataa kuponywa. Waasi hao ndio wale ‘walioachiwa chumvi’ ya uharibifu wa milele.—Ufunuo 20:15.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki