-
Ugiriki—Ile Serikali Kubwa ya Tano ya UlimwenguMnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
-
-
“Yule mume wa wale mbuzi, kwa upande wake, alijishaua sana kufikia ukomo; lakini mara tu alipokwisha kuwa mwenye uweza, ile pembe kubwa ilivunjwa, na badala ya hiyo nne zikaendelea kuja juu kwa njia yenye kutokeza, kuelekea zile pepo nne za mbingu. . . . Yule mbuzi-mume anasimamia mfalme wa Ugiriki; na kwa habari ya ile pembe kubwa ambayo ilikuwa kati ya macho yake, hiyo inasimamia mfalme wa kwanza. Na hiyo ikiisha kuwa imevunjwa, hivi kwamba kulikuwa na nne ambazo mwishowe kabisa zilisimama badala yayo, kuna falme nne kutoka taifa lake ambazo zitasimama, lakini si kwa nguvu zake.”—Danieli 8:8 21, 22, NW.
-
-
Ugiriki—Ile Serikali Kubwa ya Tano ya UlimwenguMnara wa Mlinzi—1988 | Aprili 15
-
-
Kama Biblia ilivyotabiri, mshangilio wa Aleksanda wa utawala wa ulimwengu ulikuwa wa muda mfupi. Akiwa kwenye kilele chenyewe cha ushindi wake, kwenye umri wa miaka 32 tu, yalikoma maushindi ya Aleksanda yasiyo na huruma. Akiwa amepatwa na homa kali ya maleria, yeye aliendelea kula karamu mpaka kulewa, na akafa kwa ghafula katika Babuloni katika 323 K.W.K. Mwili wake ulipelekwa Misri na kuingizwa kaburini katika Aleksandria. “Ile pembe kubwa” ambayo “inasimamia mfalme wa kwanza” ilikuwa imevunjwa. Halafu ni jambo gani lilipata milki yake?
Unabii ulikuwa umesema kwamba ufalme wake ungegawanywa “lakini si kwa wazao wake wa baadaye.” Philip Arrhidayo, ndugu ya Aleksanda asiyeweza mambo, alitawala kwa muda mfupi lakini akauawa. Ndivyo ilivyotukia pia kwa Aleksanda (Allou) mwana halali wa Aleksanda na Heracles (Hercules) mwana wake wa haramu. Hivyo ndivyo ulivyofifilia mbali ukoo wa Aleksanda Mkuu, yule mmwagaji-damu mkuu.
Lililotabiriwa pia lilikuwa kwamba “kuna falme nne kutoka taifa lake ambazo zitasimama, lakini si kwa nguvu zake” na kwamba ufalme wake ‘ungegawanywa kuelekea zile pembe nne za mbingu, lakini . . . si kulingana na eneo la utawala ambalo kwalo yeye alikuwa ametawala.” Je! jambo hili lilitukia?
Baada ya muda, ile milki kubwa ya Aleksanda iligawanywa miongoni mwa majemadari wake wanne: (1) Jemadari Kasanda—Makedonia na Ugiriki. (2) Jemadari Lisimako—Esia Ndogo na Thrasi ya Ulaya. (3) Jemadari Seleuko Niketa—Babulonia, Umedi, Siria, Uajemi na mikoa ya mashariki mpaka kwenye Mto Indo. (4) Jemadari Ptolemi Lago—Misri, Libya, na Palestina. Kama ilivyokuwa imesemwa kwa unabii, kutokana na ufalme mkuu mmoja wa Aleksanda zilitokea falme nne za Kiheleni, au zilizogirikishwa.a
-