-
Ni Nani Ataongoza Mataifa Kwenye Amani?Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
-
-
18 Angalia maneno ya unabii kwenye Danieli 9:24, 25 (JP): “Majuma sabini yameamriwa juu ya watu wako na juu ya jiji lako takatifu, ili kumaliza ukiukaji sheria, na kufanyiza mwisho wa dhambi, na kusamehe makosa, na kuleta ndani uadilifu wa milele . . . mpaka kwa yule mpakwa-mafuta [“Mesiya,” Kiebrania, Ma·shiʹach], mkuu.” Mtu hawezi kuepuka kuona ufungamano uliowekwa katika andiko hilo kati ya “Mesiya” (Mpakwa-Mafuta) na ‘kumalizwa kwa ukiukaji sheria na kufanyiza mwisho wa dhambi.’ Mstari wa 26 huendelea kutaarifu kwamba “baada ya majuma sitini na mawili mpakwa-mafuta [“Mesiya,” Kiebrania Ma·shiʹach] atakatiliwa mbali,” yaani, auawe. (Ona kisanduku, ‘Mpakwa-Mafuta’ Alikuwa Nani? Angekuja Wakati Gani?”)
-
-
Ni Nani Ataongoza Mataifa Kwenye Amani?Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
-
-
20 Kwa sababu hizo zilizo juu, fundisho la kwamba kifo cha Mesiya kingewezesha msamaha kamili wa dhambi machoni pa Mungu lilieleweka kwa urahisi na Wayahudi wengi wa karne ya kwanza. Walijua kwamba Maandiko yalisema juu ya kutokamilika kwa mwanadamu kulikorithiwa. (Mhubiri 7:20) Uhitaji wa dhabihu ili kufunika dhambi ulikuwa somo lililotambuliwa kila siku; ulidokezwa waziwazi katika mpango na namna yenyewe ya agano la Sheria. Matukio yaliyoelezwa katika masimulizi ya maisha ya Yesu humwonyesha akiwa mwanadamu mkamilifu ambaye kifo chake kingeweza kuleta ufuniko wa dhambi ya ainabinadamu.f (Mathayo 20:28; Luka 1:26-38) Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yalipokazia kwamba dhabihu mbalimbali chini ya Sheria zilifananisha dhabihu hiyo moja kamilifu na ya mwisho, maana kamili zaidi ilitolewa kwa mpango mzima wa Sheria, pamoja na sehemu nyingine za Maandiko.g—Waebrania 10:1-10.
-
-
Ni Nani Ataongoza Mataifa Kwenye Amani?Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
-
-
f Mtume Paulo alirejezea Yesu kuwa ‘Adamu wa pili,’ ambaye kifo chake kilileta kufunikwa kwa dhambi iliyorithiwa kutoka Adamu. (1 Wakorintho 15:45-47; Warumi 5:12, 15-19) Kwa habari zaidi juu ya kwa nini mpango kama huo ulihitajiwa, ona sehemu ya “Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Ainabinadamu?,” mafungu , na na kielezi-chini.
-