Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ni Nani Ataongoza Mataifa Kwenye Amani?
    Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
    • 18 Angalia maneno ya unabii kwenye Danieli 9:24, 25 (JP): “Majuma sabini yameamriwa juu ya watu wako na juu ya jiji lako takatifu, ili kumaliza ukiukaji sheria, na kufanyiza mwisho wa dhambi, na kusamehe makosa, na kuleta ndani uadilifu wa milele . . . mpaka kwa yule mpakwa-mafuta [“Mesiya,” Kiebrania, Ma·shiʹach], mkuu.” Mtu hawezi kuepuka kuona ufungamano uliowekwa katika andiko hilo kati ya “Mesiya” (Mpakwa-Mafuta) na ‘kumalizwa kwa ukiukaji sheria na kufanyiza mwisho wa dhambi.’ Mstari wa 26 huendelea kutaarifu kwamba “baada ya majuma sitini na mawili mpakwa-mafuta [“Mesiya,” Kiebrania Ma·shiʹach] atakatiliwa mbali,” yaani, auawe. (Ona kisanduku, ‘Mpakwa-Mafuta’ Alikuwa Nani? Angekuja Wakati Gani?”)

      ‘MPAKWA-MAFUTA’ ALIKUWA NANI? ANGEKUJA WAKATI GANI?

      Danieli 9:24 (JP): “Majuma sabini yameamriwa juu ya watu wako.”

      Ni nini kusudi la kipindi hicho cha wakati kilichotajwa?

      “Kufanyiza mwisho wa dhambi, na kusamehe makosa, na kuleta ndani uadilifu wa milele na kutia muhuri njozi na nabii.” Kutokana na maneno hayo pekee, mtu angetarajia huu uwe mmojawapo unabii wa maana zaidi katika Maandiko.

      Danieli 9:26 (JP): “Baada ya majuma sitini na mawili mpakwa-mafuta [“Mesiya,” Kiebrania Ma·shiʹach] atakatiliwa mbali, asiwepo tena.” Angalia kwamba kukatiliwa mbali, au kifo cha Mesiya, kingetukia kabla ya uharibifu wa hekalu la pili katika 70 W.K., kama vile mstari huo uendeleavyo kusema: “Na watu wa mkuu ambao watakuja wataharibu lile jiji na patakatifu.”

      Waelezaji wa Kiyahudi huelewaje unabii huo?

      Hakuna fasiri yenye kiwango kimoja, ambayo imekubaliwa kwa unabii huo kwa upande wa waelezaji wa Kiyahudi. Baadhi yao hujaribu kuhusisha sehemu zao na kule kurudi kutoka katika uhamisho wa Kibabuloni (537 K.W.K.), wengine na kipindi cha uasi wa Wamakabayo dhidi ya majeshi ya Wagiriki (168-165 K.W.K.), na wengine na uharibifu wa hekalu la pili na Waroma katika 70 W.K., hali wengine huhusisha sehemu za unabii huo na kuja kwa Mesiya kwa wakati ujao.

      Kwa ujumla mtu angeweza kusema kwamba fasiri za kisasa za Kiyahudi hupungukiwa katika mambo mawili ya msingi:

      1. Fasiri hizo huelekea kupunguza umaana wa unabii huo, zikipuuza kabisa kusudi lao lililosemwa waziwazi la kuleta mwisho wa dhambi na uovu na kuanzisha uadilifu wa milele.

      2. Hakuna yoyote ya mafafanuzi hayo yaliyokubaliwa inayofaana kwa usahihi na uhesabu wowote ufaao wa wakati, jambo lililokuwa hasa ndilo kusudi la kumpa Danieli unabii huo kwa namna ambayo ingeweza kutumiwa kujua wakati ambapo utimizo huo ungetukia.—Linganisha Danieli 9:2.

      Je! kuna ufafanuzi wa unabii huo ambao hupatana na kusudi lao lililosemwa waziwazi na pia na matukio hakika ya kihistoria?

      Angalia yafuatayo:

      Majuma sabini: Waelezaji wa Kiyahudi karibu wote huelewa hayo yakimaanisha majuma ya miaka, yaani, miaka 490. Hilo lapatana na hesabu ya kiunabii ya Kimaandiko kwa “mwaka mmoja kwa kila siku moja.”—Hesabu 14:34; Mambo ya Walawi 25:8; Ezekieli 4:6.

      “Tangu kutolewa kwa lile neno la kurudisha na kujenga Yerusalemu” (Danieli 9:25, JP): Nehemia husimulia kwamba katika mwaka wa 20 wa Mfalme Artasaksi, alipewa utume wa kurudisha na kujenga upya Yerusalemu. Hiyo ilikuwa katika mwaka 455 K.W.K.—Nehemia 2:1-8; ona Insight on the Scriptures, Buku 2, kurasa 614-16, 899-900, kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

      Majuma saba: Majuma saba (ya miaka, au miaka 49) huhusiana na kipindi cha kukamilisha kurudishwa kwa jiji, Yerusalemu.

      Majuma sitini na mawili: Majuma sitini na mawili (ya miaka, au miaka 434) huhusiana na kile kipindi cha baada ya kukamilishwa kwa jiji mpaka kuja kwa yule Mesiya.i

      Kwa kujumlisha vipindi hivyo viwili vya wakati pamoja, mtu hufikia majuma 69 ya miaka, au miaka 483. Kuhesabu kutoka mahali pa kuanzia pa 455 K.W.K. huonyesha mwisho wa juma la 69 kuwa 29 W.K.

      29W.K.: Myahudi aitwaye Yesu (Kiebrania, Yeshua), aliyezaliwa katika Bethlehemu na kulelewa katika Nazareti, kutoka nasaba ya Daudi, aanza kuhubiri kotekote katika nchi ya Israeli.—Luka 3:1-3, 21, 22.

      “Na baada ya yale majuma sitini na mawili Mesiya atakatiliwa mbali” (Danieli 9:26, NW): Katika mwaka 33 W.K., Yesu auawa, baada ya kuhubiri kwa miaka mitatu na nusu. Hiyo yalingana na jambo ambalo Danieli 9:27 hutaarifu.

      “Atasababisha dhabihu na zawadi za matoleo kukoma” (Danieli 9:27, NW): Yesu alisema juu ya kifo chake kuwa ni dhabihu. (Mathayo 20:28) Kilileta machoni pa Mungu mwisho wa dhabihu zilizotolewa chini ya agano la Sheria. (Waebrania 8:1-13) Kifo cha Yesu cha dhabihu kiliandaa msingi wa yale yote yaliyotajwa katika Danieli 9:24.

      Kingeleta msamaha wa dhambi.

      Kilithibitisha ahadi na unabii mwingi wa Mungu kuwa kweli.

      Kiliandaa msingi halali kulingana na viwango vya Mungu kwa uadilifu wa milele katika wakati ujao.

      Yote hayo yalitimia, kama unabii ulivyoonyesha, kabla ya uharibifu wa hekalu la pili.

      Je! ufafanuzi mwingine wowote wenye kuonyesha utimizo wa wakati uliopita usingekosa kusudi lililosemwa waziwazi?

      Kuelekeza utimizo wa unabii huo kwenye wakati ujao, kungeuondoa mbali sana na kipindi cha wakati wao kilichotolewa cha majuma 70 ya miaka, na utimizo huo haungekuwa kabla ya uharibifu wa hekalu la pili la Yerusalemu.

      i Zile alama za vituo zipatikanazo katika maandishi-awali ya Kiebrania cha kisasa (maandishi-awali ya Kiebrania cha awali hayakuwa na nukta za irabu au alama za vituo), ambazo husababisha uelewevu tofauti wa ugawanyaji huu wa wakati, si za awali bali ni nyongeza ya waandishi katika zile Enzi za Katikati ambao kwa wazi walifanya hivyo kwa kuwa fasiri ya andiko hilo ilionekana kuwa ilitimizwa katika Yesu.

  • Ni Nani Ataongoza Mataifa Kwenye Amani?
    Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
    • 20 Kwa sababu hizo zilizo juu, fundisho la kwamba kifo cha Mesiya kingewezesha msamaha kamili wa dhambi machoni pa Mungu lilieleweka kwa urahisi na Wayahudi wengi wa karne ya kwanza. Walijua kwamba Maandiko yalisema juu ya kutokamilika kwa mwanadamu kulikorithiwa. (Mhubiri 7:20) Uhitaji wa dhabihu ili kufunika dhambi ulikuwa somo lililotambuliwa kila siku; ulidokezwa waziwazi katika mpango na namna yenyewe ya agano la Sheria. Matukio yaliyoelezwa katika masimulizi ya maisha ya Yesu humwonyesha akiwa mwanadamu mkamilifu ambaye kifo chake kingeweza kuleta ufuniko wa dhambi ya ainabinadamu.f (Mathayo 20:28; Luka 1:26-38) Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yalipokazia kwamba dhabihu mbalimbali chini ya Sheria zilifananisha dhabihu hiyo moja kamilifu na ya mwisho, maana kamili zaidi ilitolewa kwa mpango mzima wa Sheria, pamoja na sehemu nyingine za Maandiko.g—Waebrania 10:1-10.

  • Ni Nani Ataongoza Mataifa Kwenye Amani?
    Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?
    • f Mtume Paulo alirejezea Yesu kuwa ‘Adamu wa pili,’ ambaye kifo chake kilileta kufunikwa kwa dhambi iliyorithiwa kutoka Adamu. (1 Wakorintho 15:45-47; Warumi 5:12, 15-19) Kwa habari zaidi juu ya kwa nini mpango kama huo ulihitajiwa, ona sehemu ya “Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Ainabinadamu?,” mafungu , na na kielezi-chini.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki