-
“Mfalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa MwishoMnara wa Mlinzi (Funzo)—2020 | Mei
-
-
13. Mfalme wa kaskazini alifanya nini katika miaka ya 1930 na wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu?
13 Kisha, katika miaka ya 1930 na hasa wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu, mfalme wa kaskazini aliwashambulia watu wa Mungu bila huruma. Halafu chama cha Nazi kilipochukua mamlaka nchini Ujerumani, Hitler na wafuasi wake walipiga marufuku kazi ya watu wa Mungu. Wapinzani hao waliwaua mamia ya watu wa Yehova na kuwapeleka maelfu zaidi kwenye kambi za mateso. Danieli alikuwa ametabiri kuhusu matukio hayo. Mfalme wa kaskazini alifanikiwa ‘kupachafua patakatifu’ na “kuondoa ile dhabihu inayotolewa daima” kwa kuwawekea watu wa Mungu vizuizi vikali ili wasilisifu jina la Yehova hadharani. (Dan. 11:30b, 31a) Hata Hitler aliyekuwa kiongozi wao aliapa kuwafutilia mbali watu wa Mungu nchini Ujerumani.
-
-
“Mfalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa MwishoMnara wa Mlinzi (Funzo)—2020 | Mei
-
-
USHIRIKIANO USIO WA KAWAIDA
17. ‘Kile kitu chenye kuchukiza sana kinachosababisha ukiwa’ ni nini?
17 Mfalme wa kaskazini amemuunga mkono mfalme wa kusini katika jambo moja muhimu; ‘walisimamisha kile kitu chenye kuchukiza sana kinachosababisha ukiwa.’ (Dan. 11:31) ‘Kitu hicho chenye kuchukiza sana’ ni shirika la Umoja wa Mataifa.
18. Kwa nini shirika la Umoja wa Mataifa linatajwa kuwa ‘kitu chenye kuchukiza sana’?
18 Shirika la Umoja wa Mataifa linatajwa kuwa ‘kitu chenye kuchukiza sana’ kwa sababu linadai kwamba linaweza kufanya jambo ambalo Ufalme wa Mungu pekee ndio unaoweza kufanya, yaani, kuleta amani duniani. Na unabii wa Danieli unataja kwamba kitu hicho chenye kuchukiza sana ‘kinasababisha ukiwa’ kwa sababu shirika la Umoja wa Mataifa litashambulia dini zote za uwongo na kuziangamiza.—Tazama chati “Wafalme Wanaopingana Katika Wakati wa Mwisho.”
-