Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Alijifunza Kutokana na Makosa Yake
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
    • Lakini ngoja kidogo! Aliona kitu kikisonga karibu naye, kitu kikubwa, cheusi, kilicho hai. Kilizidi kumkaribia. Mdomo mkubwa ulifunguka na kummeza!

      Huu ndio mwisho. Hata hivyo, Yona alishangazwa na jambo moja. Bado alikuwa hai! Hakuwa amevunjwa-vunjwa, wala kumeng’enywa, wala kusongwa pumzi. Ingawa ni kana kwamba alikuwa katika kaburi lake, bado alikuwa hai. Pole kwa pole, Yona alijawa na woga wenye heshima. Bila shaka, ni Mungu wake, Yehova, ‘aliyemweka samaki mkubwa ammeze Yona.’c—Yona 1:17.

      Dakika zilizidi kupita. Akiwa humo, katika giza kubwa zaidi ambalo amewahi kuona, Yona alipata nafasi ya kutafakari na kusali kwa Yehova Mungu. Sala yake, ambayo yote imerekodiwa katika sura ya pili ya Yona, inafunua mambo mengi. Inaonyesha kwamba Yona alikuwa na ujuzi mwingi wa Maandiko, kwa sababu inarejelea Zaburi mara nyingi. Pia, inaonyesha sifa fulani nzuri ya Yona: alikuwa mwenye shukrani. Yona alimalizia sala yake hivi: “Lakini mimi, kwa sauti ya kutoa shukrani nitakutolea dhabihu. Nilichoweka nadhiri, nitakitimiza. Wokovu ni wa Yehova.”—Yona 2:9.

      Yona alijifunza kwamba Yehova anaweza kumwokoa mtu yeyote, mahali popote, wakati wowote. Hata humo, “ndani ya tumbo la samaki huyo,” Yehova alimpata na kumwokoa mtumishi wake aliyekuwa taabani. (Yona 1:17) Ni Yehova peke yake ambaye angeweza kumhifadhi mtu hai kwa siku tatu mchana na usiku ndani ya tumbo la samaki mkubwa. Leo, tunafaa kukumbuka kwamba ‘pumzi yetu imo mkononi mwa’ Yehova Mungu. (Danieli 5:23) Tuko hai kwa sababu ya mapenzi yake. Je, tunaonyesha kwamba tunashukuru? Basi, je, hatupaswi kumtii Yehova?

      Namna gani Yona? Je, alijifunza kumwonyesha Yehova shukrani kwa kumtii? Ndiyo. Baada ya kukaa siku tatu mchana na usiku, samaki huyo alimpeleka Yona hadi ufuoni na “akamtapika Yona kwenye nchi kavu.” (Yona 2:10) Hebu fikiria—baada ya kupitia mambo hayo yote, Yona hakuhitaji hata kuogelea! Bila shaka, alihitaji kutafuta njia ya kutoka ufuo huo ambao samaki alimwacha. Hata hivyo, baada ya muda mfupi roho yake ya kuonyesha shukrani ilijaribiwa. Yona 3:1, 2 inasema: “Ndipo neno la Yehova likamjia Yona mara ya pili, na kusema: ‘Ondoka, uende Ninawi lile jiji kubwa, ukalitangazie neno ninalokuambia.’” Yona angefanya nini?

  • Alijifunza Kutokana na Makosa Yake
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
    • c Neno la Kiebrania “samaki,” lilitafsiriwa katika Kigiriki kuwa “mnyama mkubwa wa baharini,” au “samaki mkubwa.” Ingawa hakuna njia ya kuthibitisha ni kiumbe gani wa baharini anayetajwa, imegunduliwa kwamba katika Bahari ya Mediterania kuna papa wakubwa wanaoweza kummeza mtu mzima. Kuna papa wakubwa zaidi katika maeneo mengine. Kwa mfano, papa-nyangumi anaweza kukua kufikia urefu wa mita 15 au zaidi!

  • Alijifunza Kutokana na Makosa Yake
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
    • Hata bila Mungu kuingilia kati, nyakati nyingine mambo ya ajabu yanatokea. Kwa mfano, inasemekana kwamba mnamo 1758, baharia mmoja alianguka ndani ya Bahari ya Mediterania kutoka melini na akamezwa na papa. Hata hivyo, papa huyo alipigwa kwa mzinga. Papa huyo alimtema baharia huyo na akaokolewa akiwa hai bila majeraha makubwa. Ikiwa kwa kweli jambo hilo lilitendeka, tunaweza kusema hilo lilikuwa jambo la ajabu, au hata la kustaajabisha, lakini si muujiza. Je, Mungu hangaliweza kutumia nguvu zake kufanya mambo makubwa hata zaidi?

      Pia, wachambuzi wanasema kwamba hakuna mtu anayeweza kuendelea kuwa hai ndani ya samaki kwa siku tatu bila kusongwa pumzi. Hata hivyo, wanadamu wametumia akili sana hivi kwamba wamegundua jinsi ya kujaza hewa iliyoshindiliwa ndani ya matangi na kuitumia kupumua chini ya maji kwa muda mrefu. Je, Mungu hangaliweza kutumia nguvu na hekima yake isiyo na kifani ili kuhakikisha Yona anaendelea kuwa hai na kupumua kwa siku tatu? Kama tu malaika wa Yehova alivyomwambia Maria, mama ya Yesu, “kwa Mungu hakuna tangazo lolote lisilowezekana.”—Luka 1:37.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki