Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Tangazeni Mambo Haya Kati ya Mataifa”
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
    • 8. Kwa nini “mabaki ya Yakobo” wanalinganishwa na simba?

      8 Katika ujumbe wa nabii Mika, wale wanaotoa ‘ng’ombe-dume wachanga wa midomo yao’ wanalinganishwa na simba. Aliandika hivi: “Mabaki ya Yakobo watakuwa kati ya mataifa . . . kama simba katikati ya wanyama wa msituni, kama mwana-simba mwenye manyoya shingoni katikati ya makundi ya kondoo, ambaye, anapopita kati, hukanyaga-kanyaga na pia hurarua vipande-vipande; wala hakuna mkombozi.” (Mika 5:8) Kwa nini anawalinganisha na simba? Leo, watu wa Mungu, wakiongozwa na mabaki watiwa-mafuta, lazima waonyeshe ujasiri kama wa simba wanapoyatangazia mataifa ujumbe wenye kuonya.a

      Picha katika ukurasa wa 169

      Je, unaitangaza siku ya Yehova kwa ujasiri?

      9. (a) Ni wakati gani unapohitaji kuwa na ujasiri kama simba? (b) Unaweza kupataje ujasiri unapokabili upinzani au kutopendezwa?

      9 Je, una ujasiri kama wa simba unapotangaza ujumbe huo wenye onyo? Huenda ukahitaji ujasiri huo unaposimama mbele ya watu wenye mamlaka, hali kadhalika unapozungumza na marika zako shuleni, kazini au unapozungumza na watu wako wa ukoo ambao si waamini. (Mika 7:5-7; Mathayo 10:17-21) Unaweza kupataje ujasiri unapokabili upinzani au kutopendezwa? Hebu sikiliza jinsi Mika alivyoweza kutimiza kazi ngumu ya kuonya kuhusu uharibifu wa Samaria na Yerusalemu: “Nimejaa nguvu, kwa roho ya Yehova, na ya haki na uwezo, ili nimwambie Yakobo maasi yake na Israeli dhambi yake.” (Mika 1:1, 6; 3:8) Wewe pia unaweza ‘kujaa nguvu’ kwa sababu wewe pia unaweza kupokea kiasi kikubwa cha roho ya Mungu yenye kutia nguvu. (Zekaria 4:6) Kwa kumtegemea Mungu katika sala, utaweza kutangaza maneno yake yanayoweza kufanya masikio yawashe.—2 Wafalme 21:10-15.

  • “Tangazeni Mambo Haya Kati ya Mataifa”
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
    • a Huenda unabii huo ulitimizwa mara ya kwanza katika enzi ya Wamakabayo wakati ambapo Wayahudi waliokuwa chini ya uongozi wa Wamakabayo walipowafukuza adui zao kutoka Yuda na kuliweka hekalu wakfu tena. Hilo liliwawezesha mabaki ya Wayahudi kumkaribisha Masihi alipotokea.—Danieli 9:25; Luka 3:15-22.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki