-
Samehe Kutoka Katika Moyo WakoMnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 15
-
-
15, 16. (a) Mika alimfafanuaje Yehova? (b) Inamaanisha nini kwamba Mungu ‘anaachilia kosa’?
15 Tusisahau kwamba Mungu ndiye kielelezo chetu katika kusamehe. (Waefeso 4:32–5:1) Kuhusu kielelezo cha Mungu cha kuachilia kosa, nabii Mika aliandika: “Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? hashiki hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema.”—Mika 7:18.
16 Kwa kumfafanua Yehova kuwa mwenye ‘kuachilia kosa,’ Biblia haisemi kwamba yeye hawezi kuyasahau makosa, kwa njia fulani akisahau makosa mengine. Fikiria visa vya Samsoni na Daudi, wote wawili walifanya makosa mazito. Mungu aliweza kuzikumbuka dhambi hizo muda mrefu baadaye; na hata sisi twajua baadhi ya dhambi zao kwa sababu Yehova alifanya ziandikwe katika Biblia. Na bado, Mungu wetu mwenye kusamehe aliwaonyesha rehema, akiwataja kuwa vielelezo vya imani tunaopaswa kuiga.—Waebrania 11:32; 12:1.
17. (a) Ni hali gani iwezayo kutusaidia kuachilia makosa ya wengine? (b) Tukijaribu kufanya hivyo, tutakuwa tukimwigaje Yehova? (Ona kielezi-chini.)
17 Naam, Yehova aliweza ‘kuyaachilia’a makosa, kama ambavyo Daudi alimwomba tena na tena ayaachilie. (2 Samweli 12:13; 24:10) Je, tunaweza kumwiga Mungu katika jambo hilo, kwa kuwa tayari kuachilia mambo yenye kuudhi na makosa ambayo watumishi wenzetu wanafanya wakiwa wanadamu wasiokamilika? Ebu wazia ukiwa katika ndege inayoondoka kwenye uwanja. Unapotazama nje, karibu na njia ya ndege unaona mtu unayemfahamu akitoa nje ulimi wake kwa njia ya kitoto yenye kuudhi. Unajua kwamba alikuwa amekasirika na huenda ni wewe anayekufanyia dhihaka hiyo. Au huenda hata si wewe anayekufikiria. Hata hivyo, ndege hiyo izungukapo ikipaa juu, unapita juu sana ya mwanamke yule, ambaye sasa anaonekana kama doa tu. Baada ya muda wa saa moja uko umbali wa mamia ya kilometa, na tayari umesahau kabisa dhihaka yake. Vivyo hivyo, mara nyingi tutasaidiwa kusamehe tukijaribu kuiga Yehova na kuliachilia kosa hilo kwa hekima. (Mithali 19:11) Je, kosa hilo halitaonekana kuwa jambo dogo sana miaka kumi ijayo au miaka mia mbili katika Milenia? Mbona usiliachilie tu?
-
-
Samehe Kutoka Katika Moyo WakoMnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 15
-
-
a Msomi mmoja asema kwamba neno la kitamathali la Kiebrania lililotumiwa katika Mika 7:18 “limetokana na tabia ya msafiri ambaye anapita bila kuona kitu ambacho hataki kukifikiria. Halimaanishi kwamba Mungu haoni dhambi, wala kwamba anaiona kuwa jambo dogo au lisilo muhimu, bali kwamba haioni katika visa fulani hususa ili atoe adhabu; kwamba hatoi adhabu, bali asamehe.”—Waamuzi 3:26; 1 Samweli 16:8.
-