Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hakuna Kitu Kinachoweza “Kututenga na Upendo wa Mungu”
    Mkaribie Yehova
    • 19 Yehova ana hisia-mwenzi. Hisia-mwenzi ni nini? Mkristo mmoja mwaminifu ambaye ni mzee kwa umri alisema: “Hisia-mwenzi ni kuhisi uchungu wako moyoni mwangu.” Je, kweli Yehova anaumizwa na uchungu wetu? Twasoma hivi kuhusu mateso ya watu wake wa taifa la Israeli: “Katika mateso yao yote yeye aliteswa.” (Isaya 63:9) Yehova hakuona tu taabu zao; bali alihisi uchungu kwa sababu ya taabu zao. Maneno ambayo Yehova aliwaambia watumishi wake yanaonyesha jinsi anavyohisi: “Anayewagusa nyinyi anagusa mboni ya jicho langu.”b (Zekaria 2:8, BHN) Mtu huhisi maumivu makali sana anapoguswa mboni ya jicho. Ndiyo, Yehova anahisi uchungu kwa ajili yetu. Tunapoteseka, anateseka pia.

  • Hakuna Kitu Kinachoweza “Kututenga na Upendo wa Mungu”
    Mkaribie Yehova
    • b Tafsiri fulani zinadokeza kwamba mtu anayegusa watu wa Mungu hagusi jicho la Mungu, bali anagusa jicho lake mwenyewe au jicho la Israeli. Kosa hilo lilitokana na waandishi fulani ambao walidhani kwamba andiko hilo halimheshimu Mungu na hivyo wakalibadili. Jitihada zao zilizopotoka zilificha wingi wa hisia-mwenzi za Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki