-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
10. Mashahidi waaminifu wa Yehova watafanya nini wanapokuwa wakikanyagwa?
10 Hata wanapokuwa wakikanyagwa washikamanifu hawa hawaachi kuwa mashahidi waaminifu wa Yehova. Kwa sababu hiyo, unabii huendelea: “‘Na mimi nitafanya mashahidi wangu wawili watoe unabii siku elfu moja mia mbili na sitini wakiwa wamevalia nguo za magunia.’ Hao wanafananishwa na mizeituni miwili na vinara vya taa viwili nao wanasimama mbele za Bwana wa dunia.”—Ufunuo 11:3, 4, NW.
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
13. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba Wakristo wapakwa-mafuta walifananishwa na mashahidi wawili? (b) Ni unabii gani wa Zekaria ambao tunakumbushwa na Yohana kuwaita mashahidi wawili “mizeituni miwili na vinara vya taa viwili”?
13 Uhakika wa kwamba wao walifananishwa na mashahidi wawili unatuthibitishia kwamba ujumbe wao ni sahihi na una msingi mzuri. (Linga Kumbukumbu 17:6; Yohana 8:17, 18.) Yohana anawaita “mizeituni miwili na vinara vya taa viwili,” akisema kwamba wao “wanasimama mbele za Bwana wa dunia.” Hili ni rejezo la wazi kwenye unabii wa Zekaria, ambaye aliona kinara cha taa chenye matawi saba na mizeituni miwili. Hiyo mizeituni ilisemekana kuwa ni picha ya “wapakwa-mafuta wawili,” yaani, Gavana Zerubabeli na Kuhani Mkuu Yoshua, “wanasimama kando ya Bwana wa dunia kwa ujumla.”—Zekaria 4:1-3, 14, NW.
14. (a) Ni nini kilichoonyeshwa na njozi ya Zekaria ya mizeituni miwili? na kinara cha taa? (b) Wakristo wapakwa-mafuta wangepatwa na nini wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu?
14 Zekaria aliishi wakati wa kujenga upya, na njozi yake ya mizeituni miwili ilimaanisha kwamba Zerubabeli na Yoshua wangebarikiwa kwa roho ya Yehova katika kuimarisha watu kwa ajili ya kazi. Njozi ya vinara vya taa ilikumbusha Zekaria ‘asidharau siku ya vitu vidogo’ kwa sababu makusudi ya Yehova yangetimizwa—“‘si kwa kani ya kijeshi, wala kwa nguvu, bali kwa roho yangu,’ Yehova wa majeshi amesema.” (Zekaria 4:6, 10; 8:9, NW) Kile kikosi kidogo cha Wakristo kilichodumu katika kupelekea aina ya binadamu nuru ya ukweli wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu kingetumiwa jinsi iyo hiyo katika kazi ya kujenga upya. Wao pia wangekuwa chanzo cha kitia-moyo na, wajapokuwa wachache, wangejifunza kutegemea imara ya Yehova, wasidharau siku ya mianzo midogo.
-