-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
2. Katika mfano wa Yesu wa ngano na magugu, mbegu nzuri inafananisha nani?
2 Hata hivyo, mfano mmoja ambao Yesu alitoa unakazia kazi ya kuwakusanya wale watakaotawala pamoja naye katika Ufalme wake. Kwa kawaida, mfano huo unaitwa mfano wa ngano na magugu na unapatikana katika sura ya 13 ya kitabu cha Mathayo. Ingawa katika mfano mwingine Yesu anatuambia kwamba mbegu ambayo inapandwa ni “neno la ufalme,” katika mfano huu, anatuambia kwamba mbegu hiyo nzuri inafananisha jambo lingine tofauti, inafananisha “wana wa ufalme.” (Mt. 13:19, 38) Hao si raia wa Ufalme bali ni “wana,” au warithi wa Ufalme.—Rom. 8:14-17; soma Wagalatia 4:6, 7.
-
-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
4. (a) Mtu anayetajwa katika mfano huo ni nani? (b) Yesu alianza wakati gani na jinsi gani kupanda mbegu hiyo?
4 Mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake ni nani? Yesu anajibu swali hilo baadaye anapowaeleza hivi wanafunzi wake: “Mpandaji wa mbegu nzuri ni Mwana wa binadamu.” (Mt. 13:37) Yesu, ambaye ni “Mwana wa binadamu,” alitayarisha shamba katika kipindi cha miaka mitatu na nusu ya huduma yake duniani ili apande mbegu. (Mt. 8:20; 25:31; 26:64) Kisha kuanzia Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K. na kuendelea, alianza kupanda mbegu nzuri, yaani, “wana wa ufalme.” Inaonekana kwamba mbegu hiyo ilipandwa wakati Yesu, akiwa mwakilishi wa Yehova, alipoanza kuwamwagia wanafunzi wake roho takatifu, na hivyo akawatia mafuta ili wawe wana wa Mungu.b (Mdo. 2:33) Mbegu hiyo nzuri ilikomaa na kuwa ngano. Kwa hiyo, Yesu alipanda mbegu nzuri ili mwishowe akusanye hesabu kamili ya wale ambao wangekuwa warithi na watawala wenzake katika Ufalme wake.
-
-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
5. Adui anayetajwa katika mfano huo ni nani, na magugu yanafananisha nani?
5 Adui ni nani, na magugu ni nani? Yesu anatuambia kwamba adui “ni Ibilisi.” Biblia inasema magugu ni “wana wa yule mwovu.” (Mt. 13:25, 38, 39) Kwa njia halisi, magugu ambayo Yesu alizungumzia huenda yalikuwa magugu fulani yenye sumu ambayo yanafanana sana na ngano ambayo haijakomaa. Mfano huo unawafaa sana Wakristo wa uwongo, wale wanaodai kuwa wana wa Ufalme lakini hawazai matunda yanayofaa! Wakristo hao wenye unafiki ambao wanadai kuwa wafuasi wa kweli wa Kristo kwa kweli wao ni sehemu ya “mbegu” ya Shetani Ibilisi.—Mwa. 3:15.
-
-
“Waadilifu Watang’aa kwa Uangavu Kama Jua”Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
7. Je, ngano iligeuka na kuwa magugu? Eleza.
7 Yesu hakusema kwamba ngano ingegeuka na kuwa magugu, alisema kwamba magugu yangepandwa katikati ya ngano. Kwa hiyo, mfano huo haumaanishi kwamba Wakristo wa kweli wangeacha kweli. Badala yake, unaonyesha kwamba Shetani angejitahidi kwa makusudi kulipotosha kutaniko la Kikristo kwa kuingiza watu waovu ndani yake. Mtume wa mwisho, Yohana, alipokuwa amezeeka, uasi-imani huo ulikuwa unaonekana waziwazi.—2 Pet. 2:1-3; 1 Yoh. 2:18.
-