Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Watu Wanaohubiri​—Wahudumu Wanajitoa kwa Hiari
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
    • Mwanamume aliyepata hazina iliyofichwa uwanjani

      Kama mwanaume anayepata hazina iliyofichwa anavyojawa na shangwe, Wakristo hufurahi kwamba wamepata kweli ya Ufalme (Ona fungu la 20)

      20. Mfano wa Yesu kuhusu hazina iliyofichwa unaonyeshaje kwamba wafuasi wake wangetii shauri lake la kuendelea kuutafuta kwanza Ufalme?

      20 Yesu alijua jinsi ambavyo wafuasi wake wangetii shauri la kuutafuta kwanza Ufalme. Fikiria mfano wake wa hazina iliyofichwa. (Soma Mathayo 13:44.) Anapofanya kazi zake za kawaida shambani, mtu anayetajwa katika mfano huo anapata hazina iliyofichwa na mara moja anatambua thamani yake. Anafanya nini? “Kwa sababu ya shangwe aliyo nayo, anaenda na kuuza vitu alivyo navyo na kulinunua shamba hilo.” Tunajifunza nini? Tunapopata kweli ya Ufalme na kutambua thamani yake, kwa shangwe tutadhabihu jambo lolote lile ili kutanguliza mambo ya Ufalme maishani mwetu.d

  • Watu Wanaohubiri​—Wahudumu Wanajitoa kwa Hiari
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
    • d Yesu alifundisha jambo hilohilo katika mfano wake kuhusu mwanabiashara anayesafiri kutafuta lulu moja ya thamani kubwa. Anapoipata, mwanabiashara huyo anauza vitu vyote alivyo navyo na kuinunua. (Mt. 13:45, 46) Pia, mifano yote miwili inatufundisha kwamba tunaweza kujifunza kweli ya Ufalme katika njia mbalimbali. Wengine hupata kweli hiyo bila kutarajia; hali wengine huitafuta. Lakini hata iwe tulipata kweli kwa njia gani, tuko tayari kujidhabihu ili tuutangulize Ufalme maishani.

  • Watu Wanaohubiri​—Wahudumu Wanajitoa kwa Hiari
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki