-
Mfalme Anawasafisha Watu Wake KirohoUfalme wa Mungu Unatawala!
-
-
Wavu wa kukokota unawakilisha kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme kwa wanadamu wote ambao wanafananishwa na bahari (Ona fungu la 18)
18 Kushusha “wavu wa kukokota . . . ndani ya bahari.” Wavu wa kukokota unawakilisha kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme kwa wanadamu wote ambao wanafananishwa na bahari. “Kukusanya samaki wa kila aina.” Habari njema inawavutia watu wa aina zote—wale wanaochukua hatua na kuwa Wakristo wa kweli, na pia wengi ambao mwanzoni wanaweza kuonyesha kwamba wanapendezwa lakini hawachukui msimamo upande wa ibada safi.e Kukusanya “walio wazuri ndani ya vyombo.” Wanyofu wanakusanywa kwenye makutaniko yanayofananishwa na vyombo, ambamo wanaweza kumtolea Yehova ibada safi. Kuwatupilia mbali samaki “wasiofaa.” Katika kipindi chote cha siku za mwisho, Kristo na malaika wamekuwa wakitenganisha “waovu kutoka katikati ya waadilifu.”f Matokeo ni kwamba wote ambao hawana mioyo minyofu, yaani, wale ambao huenda hawataki kuacha mazoea au mafundisho ya uwongo, hawajaruhusiwa kuchafua makutaniko.g
-
-
Mfalme Anawasafisha Watu Wake KirohoUfalme wa Mungu Unatawala!
-
-
f Kutenganishwa kwa samaki wazuri na samaki wasiofaa ni tofauti na kutenganishwa kwa kondoo na mbuzi. (Mt. 25:31-46) Kutenganishwa kwa kondoo na mbuzi au hukumu ya mwisho, kunafanywa wakati wa dhiki kuu inayokuja. Kabla ya wakati huo, wote walio kama samaki wasiofaa wanaweza kumrudia Yehova na kukusanywa katika makutaniko yanayofananishwa vyombo.—Mal. 3:7.
-