-
“Mtu Mwingine Hajapata Kamwe Kusema Kama Huyu”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
9 Wakati mmoja, wakusanya-kodi walimuuliza Petro ikiwa Yesu analipa kodi ya hekalu.c Bila kusita Petro alijibu, “Analipa.” Baadaye, Yesu alimuuliza: “Unaonaje, Simoni? Wafalme wa dunia hupokea ushuru au kodi ya kichwa kutoka kwa nani? Kutoka kwa wana wao au kutoka kwa wageni?” Petro akajibu: “Kutoka kwa wageni.” Kisha Yesu akasema: “Basi, kwa kweli wana hawalipi kodi.” (Mathayo 17:24-27) Bila shaka, Petro alitambua kusudi la maswali hayo, kwa kuwa watu wa familia za wafalme hawakulipa kodi. Hivyo basi, kwa sababu Yesu ni Mwana mzaliwa-pekee wa Mfalme wa mbinguni aliyekuwa akiabudiwa hekaluni, hakuhitaji kulipa kodi. Ona kwamba badala ya kumwambia Petro jibu moja kwa moja, Yesu alitumia maswali kwa busara kumsaidia Petro afikie kauli sahihi na kuona uhitaji wa kufikiri kwa uangalifu kabla ya kujibu endapo hali kama hiyo itatokea tena.
-
-
“Mtu Mwingine Hajapata Kamwe Kusema Kama Huyu”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
c Kila mwaka, Wayahudi walipaswa kulipa kodi ya hekalu ya drakma mbili, zinazolingana na malipo ya kazi ya siku mbili. Kitabu kimoja kinasema: “Kodi hiyo ilitumiwa kulipia gharama za toleo la kuteketezwa la kila siku na za dhabihu zote zilizotolewa kwa ajili ya watu.”
-