-
Mchungaji AnayejaliMnara wa Mlinzi—2008 | Februari 1
-
-
Akimfananisha Yehova na mchungaji, Yesu alisema: “Mtu akiwa na kondoo 100 na mmoja apotee, je, hatawaacha wale 99 milimani na kuondoka kwenda kumtafuta yule anayepotea? Naye akimpata, hakika ninawaambia ninyi, yeye humshangilia huyo zaidi kuliko wale 99 ambao hawakupotea. Vivyo hivyo Baba yangu aliye mbinguni hatamani kwamba mmoja wa wadogo hawa aangamie.” (Mathayo 18:12-14) Acha tuone Yesu anavyofafanua vizuri jinsi Yehova anavyomjali na kumpenda kila mmoja wa waabudu Wake.
-
-
Mchungaji AnayejaliMnara wa Mlinzi—2008 | Februari 1
-
-
Akitumia mfano huo, Yesu alisema kwamba Mungu hataki “mmoja wa wadogo hawa aangamie.” Mapema, Yesu alikuwa amewaonya wanafunzi wake wasimkwaze ‘mmoja wa wale wadogo wanaomwamini.’ (Mathayo 18:6) Hivyo basi, mfano wa Yesu unatufundisha nini kumhusu Yehova? Yeye ni Mchungaji anayejali sana kila mmoja wa kondoo zake, kutia ndani ‘wale wadogo’—wale ambao huenda ulimwengu ukawaona kuwa hawana thamani. Ndiyo, machoni pa Mungu, kila mmoja wa waabudu wake ni wa pekee na wa thamani.
-