Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Unaweza Kumpata Ndugu Yako
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 15
    • Kupata Msaada wa Watu Wakomavu

      12, 13. (a) Yesu alitaja hatua gani ya pili ya kushughulikia makosa? (b) Kuna tahadhari zipi zifaazo unapochukua hatua hiyo?

      12 Je, ungependa wengine wakuachilie kwa urahisi tu ikiwa una hatia ya kutenda kosa zito? La. Kwa hiyo, Yesu alionyesha kwamba baada ya hatua ya kwanza, usiache kujaribu kumpata ndugu yako, ili kumfanya aendelee kuwa na umoja pamoja nawe na wengine katika kumwabudu Mungu ifaavyo. Yesu alitaja hatua ya pili: “Ikiwa yeye hasikilizi, chukua pamoja nawe mmoja au wawili zaidi, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila jambo lipate kuthibitishwa.”

      13 Alisema chukua “mmoja au wawili zaidi.” Yeye hakusema kwamba baada ya kuchukua hatua ya kwanza, uko huru kuongea na wengine juu ya tatizo hilo, kuongea na mwangalizi asafiriye, au kuandikia akina ndugu juu ya tatizo hilo. Hata kama una hakika kabisa kwamba kosa hilo lilifanyika, bado halijathibitishwa kabisa. Haitafaa kueneza habari za uwongo ambazo zingeweza kugeuka kuwa uchongezi kwa upande wako. (Mithali 16:28; 18:8) Lakini Yesu alisema uchukue mmoja au wawili zaidi. Kwa nini? Nao wanaweza kuwa nani?

      14. Twaweza kuchukua nani katika hatua ya pili?

      14 Unajaribu kumpata ndugu yako kwa kumsadikisha kwamba amefanya dhambi na kwa kumfanya atubu ili awe na amani pamoja nawe na pamoja na Mungu. Ili kutimiza jambo hilo, ingekuwa afadhali kama huyo “mmoja au wawili” walishuhudia kosa likifanywa. Labda walikuwapo kosa lilipofanywa, au wana habari yenye msingi mzuri juu ya jambo lililofanywa (au halikufanywa) katika suala la kibiashara. Ikiwa hakuna mashahidi kama hao, wale unaowachukua huenda wakawa wenye ujuzi wa suala linalozungumziwa na basi wanaweza kuthibitisha kama jambo lililotendeka kwa kweli ni kosa. Isitoshe, ikihitajiwa baadaye, wao wanaweza kuwa mashahidi wa jambo lililosemwa, wakithibitisha mambo yaliyosemwa na jitihada iliyofanywa. (Hesabu 35:30; Kumbukumbu la Torati 17:6) Basi hao si watu wasiohusika tu, waamuzi; lakini, kuwapo kwao ni kusaidia kumpata ndugu yako na ndugu yao.

      15. Kwa nini wazee Wakristo wanaweza kusaidia ikiwa ni lazima tuchukue hatua ya pili?

      15 Usifikiri kwamba wale unaowachukua ni lazima wawe wazee kutanikoni. Lakini, wanaume wakomavu ambao ni wazee wanaweza kuchangia kwa sababu ya sifa zao za kiroho. Wazee kama hao ni “kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.” (Isaya 32:1, 2) Wao wana ujuzi wa kusababu na akina ndugu na dada na kuwarekebisha. Na mkosaji ana sababu nzuri ya kuonyesha uhakika katika “zawadi zikiwa wanadamu.” c (Waefeso 4:8, 11, 12) Kuzungumzia mambo mbele ya watu wakomavu kama hao na kusali pamoja nao kwaweza kuleta mazingira mapya na kutatua suala lililoonekana kama haliwezi kutatuliwa.—Linganisha Yakobo 5:14, 15.

  • Unaweza Kumpata Ndugu Yako
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Oktoba 15
    • c Msomi mmoja wa Biblia alieleza: “Nyakati nyingine hutukia kwamba mkosaji atakuwa tayari zaidi kupokea shauri la wawili au watatu (hasa ikiwa ni watu wenye kuheshimika) kuliko la mtu mmoja, hasa ikiwa huyo ni mtu ambaye amepata kutofautiana naye kwa maoni wakati mwingine.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki