-
Kutaniko na LijengweMnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 15
-
-
10. Kulingana na Mathayo 18:15-17, matatizo mazito yalipaswa kusuluhishwa kwa njia gani?
10 Yesu alionyesha kwamba mpango huo ungekuwapo. Kumbuka simulizi la Mathayo 18:15-17, ambamo alisema kwamba nyakati fulani tatizo linaweza kutokea kati ya watu wawili wanaomtumikia Mungu, mtu mmoja anapomtendea mwingine dhambi fulani. Yule aliyekosewa angepaswa kumfikia yule mwingine na ‘kufunua kosa lake’ faraghani, wakiwa wawili tu. Ikiwa hatua hiyo haikusuluhisha tatizo hilo, mtu mmoja au wawili ambao walijua mambo yaliyotukia wangeweza kuombwa wasaidie. Namna gani ikiwa wangeshindwa kutatatua tatizo hilo? Yesu alisema: “Asipowasikiliza hao, liambie kutaniko. Ikiwa halisikilizi hata kutaniko, mwache awe kwako kama mtu wa mataifa na kama mkusanya-kodi.” Yesu aliposema hivyo, bado Wayahudi walikuwa “kutaniko la Mungu,” kwa hiyo mwanzoni maneno yake yaliwahusu.a Hata hivyo, mara tu kutaniko la Kikristo lilipoanzishwa, maagizo hayo ya Yesu yangetumika katika kutaniko la Kikristo. Hilo ni jambo lingine linaloonyesha kwamba watu wa Mungu wangekuwa na mpangilio katika kutaniko ili kutoa mwongozo na kumjenga kila Mkristo.
11. Wazee walitimiza wajibu gani katika kusuluhisha matatizo?
11 Kwa kufaa, wanaume wazee, au waangalizi wangewakilisha kutaniko katika kushughulikia au kusuluhisha matatizo au visa vya dhambi. Na hilo linapatana na sifa za kustahili za wazee zinazotajwa katika Tito 1:9. Kwa kweli, wazee hao walikuwa wanaume wasio wakamilifu, kama vile Tito ambaye alitumwa na Paulo ayatembelee makutaniko ili ‘ayarekebishe mambo yaliyokuwa na kasoro.’ (Tito 1:4, 5) Leo, wale wanaofikiriwa kuwekwa rasmi kuwa wazee ni lazima wawe wamethibitisha imani na ujitoaji wao kwa muda fulani. Hivyo, wengine kutanikoni wanakuwa na sababu nzuri ya kutegemea mwelekezo na mwongozo unaotolewa kupitia mpango huu.
-
-
Kutaniko na LijengweMnara wa Mlinzi—2007 | Aprili 15
-
-
a Msomi wa Biblia Albert Barnes alitambua kwamba agizo la Yesu la ‘kuliambia kutaniko’ lingemaanisha “wale ambao wamepewa mamlaka ya kusikiliza kesi kama hizo, yaani, wawakilishi wa kanisa, au wale wanaotenda kwa ajili yao. Katika sinagogi la Wayahudi kulikuwa na wazee ambao walikuwa waamuzi, na kesi za aina hiyo zililetwa mbele yao.”
-