-
Iga Rehema Ya Mungu LeoMnara wa Mlinzi—1991 | Aprili 15
-
-
2. Yesu alitoa shauri gani katika Mathayo 18:15-17 juu ya kushughulikia dhambi nzito?
2 Biblia inatutolea mwono-ndani katika mawazo ya Mungu, hata juu ya mambo tunayopaswa kufanya ikiwa mtu anatutenda dhambi. Yesu aliwaambia mitume wake, ambao baadaye wangekuwa waangalizi wa Kikristo, hivi: “Ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.” Kosa ambalo lilihusika hapa halikuwa dharau ya kibinafsi tu bali lilikuwa dhambi nzito, kama vile upunjaji au uchongezi. Yesu alisema kwamba ikiwa hatua hiyo haisuluhishi jambo hilo na ikiwa mashahidi wanapatikana, yule ambaye ametendwa dhambi anapaswa kwenda pamoja nao ili kuthibitisha kwamba kulikuwa na kosa. Je! hiyo ni hatua ya mwisho? Sivyo. “[Mtenda dhambi] asipowasikiliza wao, liambie kanisa [kundi, NW]; na asipolisikiliza kanisa [kundi, NW] pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru [kodi, NW].”—Mathayo 18:15-17.
3. Yesu alimaanisha nini aliposema kwamba mtenda mabaya asiyetubu angekuwa “kama mtu wa mataifa na mtoza kodi”?
3 Kwa sababu walikuwa Wayahudi, mitume wangeweza kufahamu ilivyomaanisha kumtendea mtenda dhambi kama ‘mtu wa mataifa na mtoza kodi.’ Wayahudi waliepuka ushirika pamoja na watu wa mataifa, na waliwachukia Wayahudi ambao walifanya kazi wakiwa wa-toza kodi wa Kiroma.a (Yohana 4:9; Matendo 10:28) Hivyo, Yesu alikuwa akiwashauri wafuasi wake kwamba ikiwa kundi lilimkataa mtenda dhambi, wao wangetakiwa waache kushirikiana naye. Lakini, hiyo inapatanaje na Yesu kuwa pamoja na watoza kodi nyakati fulani?
-
-
Iga Rehema Ya Mungu LeoMnara wa Mlinzi—1991 | Aprili 15
-
-
a “Watoza kodi walichukiwa na wenyeji Wayahudi wa Palestina hasa kwa sababu nyingi: (1) walikusanya pesa kwa ajili ya mamlaka ya kigeni ambayo ilimiliki bara la Israeli, hivyo kwa njia isiyo wazi, wakiwa wanaunga mkono tendo lao ovu; (2) walikuwa na sifa mbaya ya kuwa na tabia mbaya, wakiendelea kuwa matajiri kwa hasara ya wengine wa watu wao wenyewe; na (3) kazi yao iliwahusisha kwa kawaida na Wasio Wayahudi, ikiwafanya kutokuwa safi kulingana na kanuni za kidini. Dharau kwa watoza kodi inapatikana katika A[gano] J[ipya] na vichapo vya warabi pia . . . Kulingana na hivi vilivyotajwa sasa, chuki ingeenezwa hata kwa familia ya mtoza kodi.”—The International Standard Bible Encyclopedia.
-