-
‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’Mnara wa Mlinzi—1997 | Desemba 1
-
-
1. (a) Ni kwa nini huenda ikawa Petro alikuwa amefikiri kwamba alikuwa mkarimu alipodokeza kwamba tuwasamehe wengine “mpaka mara saba”? (b) Yesu alimaanisha nini aliposema kwamba twapaswa kusamehe “mpaka mara sabini na saba”?
“BWANA, ni mara ngapi ndugu yangu atafanya dhambi dhidi yangu nami nimsamehe? Mpaka mara saba?” (Mathayo 18:21) Huenda ikawa Petro alifikiri alikuwa mwenye ukarimu sana katika dokezo lake. Wakati huo, pokeo la kirabi lilisema kwamba mtu hakupaswa kutoa msamaha zaidi ya mara tatu kwa kosa lilelile.a Kisha wazia mshangao wa Petro, Yesu alipomjibu hivi: “Nakuambia, si, Mpaka mara saba, bali, Mpaka mara sabini na saba”! (Mathayo 18:22) Huko kurudia nambari saba kulikuwa sawa na kusema “kwa wakati usio dhahiri.” Kwa maoni ya Yesu, kwa kweli hakuna mipaka kwa mara ambazo Mkristo apaswa kuwasamehe wengine.
-
-
‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’Mnara wa Mlinzi—1997 | Desemba 1
-
-
a Kulingana na Talmud ya Babiloni, pokeo moja la kirabi lilitaarifu hivi: “Ikiwa mtu akiuka-sheria, mara ya kwanza, ya pili na ya tatu husamehewa, mara ya nne hasamehewi.” (Yoma 86b) Pokeo hilo lilitegemea kwa sehemu uelewevu wenye kosa wa maandiko kama Amosi 1:3; 2:6; na Ayubu 33:29.
-