-
Mfalme Anawasafisha Watu Wake KirohoUfalme wa Mungu Unatawala!
-
-
1-3. Yesu alifanya nini alipopata hekalu likichafuliwa?
YESU aliliheshimu sana hekalu la Yerusalemu kwa sababu alijua kile kilichowakilishwa na hekalu hilo. Kwa muda mrefu hekalu hilo lilikuwa kitovu cha ibada ya kweli duniani. Lakini ibada hiyo, yaani, ibada ya Mungu mtakatifu, Yehova—lazima iwe safi na takatifu. Hivyo basi, wazia jinsi Yesu alivyohisi alipokuja hekaluni Nisani 10, 33 W.K., na kupata likichafuliwa. Ni nini kilichokuwa kikifanyika hekaluni?—Soma Mathayo 21:12, 13.
2 Katika Ua wa Mataifa, wafanyabiashara wenye pupa na wale waliokuwa wakibadili pesa walikuwa wakiwapunja waabudu waliokuja kumtolea Yehova dhabihu hekaluni.a Yesu ‘aliwafukuza wale wote waliokuwa wakiuza na kununua katika hekalu, na kuzipindua meza za wale waliokuwa wakibadili pesa.’ (Linganisha na Nehemia 13:7-9.) Aliwashutumu wanaume hao wenye ubinafsi kwa kuifanya nyumba ya Baba yake kuwa “pango la wanyang’anyi.” Kwa kufanya hivyo, Yesu alionyesha kwamba aliliheshimu hekalu na kile kilichowakilishwa na hekalu hilo. Ibada ya Baba yake ilipaswa kuwa safi!
-
-
Mfalme Anawasafisha Watu Wake KirohoUfalme wa Mungu Unatawala!
-
-
a Wayahudi kutoka maeneo mengine waliokuja hekaluni walipaswa kulipia kodi ya hekalu ya kila mwaka kwa kutumia aina fulani ya sarafu, na wale waliobadili pesa waliwatoza malipo fulani ili kuwabadilishia sarafu hizo. Kwa kuongezea, huenda wageni hao walihitaji kununua wanyama kwa ajili ya kutoa dhabihu. Yesu aliwaita wafanyabiashara hao “wanyang’anyi,” labda kwa sababu walitoza malipo ya juu kupita kiasi kwa ajili ya huduma zao.
-