Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Na Tuwe na Umoja Kama Yehova na Yesu Walivyo na Umoja
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Juni
    • UPENDO NA UNYENYEKEVU HUTUSAIDIA KUSHINDA UBAGUZI

      8. Ni kanuni gani ya msingi ambayo ndiyo nguzo ya umoja wa Kikristo? Eleza.

      8 Yesu aliwafundisha wafuasi wake kanuni ya msingi ambayo ndiyo nguzo ya umoja wetu. Alisema hivi: “Nyote ni ndugu.” (Soma Mathayo 23:8, 9.) Bila shaka, sisi sote ni “ndugu” katika maana ya kwamba sote ni wazao wa Adamu. (Mdo. 17:26) Lakini kuna zaidi. Yesu alieleza kwamba wanafunzi wake ni ndugu na dada kwa sababu walitambua kwamba Yehova ndiye Baba yao wa mbinguni. (Mt. 12:50) Zaidi ya hilo, tayari walikuwa washiriki wa familia moja kubwa ya kiroho iliyounganishwa kwa upendo na imani. Ndiyo sababu katika barua walizoandika, mara nyingi mitume waliwarejelea wanafunzi wenzao kuwa ‘ndugu na dada.’—Rom. 1:13; 1 Pet. 2:17; 1 Yoh. 3:13.a

  • Na Tuwe na Umoja Kama Yehova na Yesu Walivyo na Umoja
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Juni
    • a Neno “ndugu” linaweza kutia ndani pia washiriki wa kike wa kutaniko. Paulo aliandika barua yake kwa “akina ndugu” huko Roma. Ni wazi kwamba aliwahusisha akina dada kwa kuwa aliwataja baadhi yao kwa majina. (Rom. 16:3, 6, 12) Kwa muda mrefu, gazeti la Mnara wa Mlinzi limekuwa likiwaita waamini Wakristo kuwa ‘ndugu na dada.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki