-
Unabii wa Biblia Ambao Wewe Umeona UkitimizwaBiblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
-
-
“Mwanzo wa Maumivu Makali ya Ghafula ya Taabu”
11, 12. Vita vya kwanza vya ulimwengu vilikuwaje “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu”?
11 Mistari ya mapema ya unabii wa Yesu yamalizia kwa maneno haya: “Mambo hayo yote ni mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.” Kwa hakika ndivyo ilivyokuwa kwa vita vya ulimwengu vya kwanza. Mwisho wavyo katika 1918 haukuleta amani ya muda mrefu. Baada ya muda mfupi vilifuatwa na mapigano madogo lakini makali katika Ethiopia, Libya, Hispania, Urusi, India, na mabara mengine. Kisha vikaja vita vya ulimwengu vya pili vyenye kutisha sana, ambavyo viliua wanajeshi na raia milioni 50.
12 Na zaidi, yajapokuwa mapatano ya amani na utulivu wa pindi kwa pindi katika kupigana, ainabinadamu ingali katika vita. Katika 1987 iliripotiwa kwamba vita vikubwa 81 vilikuwa vimepiganwa tangu 1960, vikiua wanaume, wanawake, na watoto 12,555,000. Mwaka 1987 uliona vita zaidi vikipiganwa kuliko katika mwaka mwingineo wote uliotangulia wa historia iliyoandikwa.1 Kuongezea hayo, matayarisho na matumizi ya kijeshi, sasa yakifikia jumla ya karibu dola 1,000,000,000,000 kila mwaka, yanaharibu uchumi wa ulimwengu.2 Kwa hakika unabii wa Yesu juu ya ‘taifa likiinuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme’ unatimizwa. Yule farasi mwekundu wa vita aendelea na mbio zake kali duniani kote. Lakini vipi juu ya sehemu ya pili ya ishara hiyo?
-
-
Unabii wa Biblia Ambao Wewe Umeona UkitimizwaBiblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
-
-
14. Ni njaa kubwa gani tangu 1914 zimetimiza unabii wa Yesu?
14 Je! yawezekana kwamba unabii huo unatimizwa leo, ambapo mabara fulani yamefikia kupata viwango vya juu vya maisha? Mtupio jicho kwa ulimwengu wote hauachi shaka lolote kwa habari ya jibu. Kihistoria, njaa kubwa zimesababishwa na vita na misiba ya asili. Basi, haishangazi kwamba karne yetu, ambayo imekuwa na misiba na vita vingi mno, imepatwa tena na tena na njaa kubwa. Sehemu nyingi za dunia zimepatwa na misiba tangu 1914. Ripoti moja yaorodhesha njaa kubwa-kubwa zaidi ya 60 tangu 1914, katika mabara yaliyotengana kama Ugiriki, Udachi, U.S.S.R., Nigeria, Chad, Chile, Peru, Bangladesh, Bengal, Kampuchea, Ethiopia, na Japan.3 Baadhi ya njaa hizo kubwa zimeendelea kwa miaka kadhaa na kusababisha mamilioni ya vifo.
-
-
Unabii wa Biblia Ambao Wewe Umeona UkitimizwaBiblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
-
-
Matetemeko ya Dunia
17. Ni tetemeko gani la dunia lenye kuleta uharibifu lililotukia mara tu baada ya 1914?
17 Katika Januari 13, 1915, vita vya ulimwengu vya kwanza vilipokuwa na miezi michache tu, tetemeko moja la dunia lilitikisa Abruzzi, Italia, na kuua watu 32,610. Msiba huo mkubwa watukumbusha kwamba vita na upungufu wa chakula wakati wa kuwapo kwa Yesu vingeandamana na kitu kingine: “Kutakuwako . . . matetemeko ya dunia mahali hapa na mahali hapa.” Kama ilivyo kwa vita na njaa kubwa, lile tetemeko la dunia la Abruzzi lilikuwa tu “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.”a
-
-
Unabii wa Biblia Ambao Wewe Umeona UkitimizwaBiblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
-
-
a Kulikuwako angalau matetemeko ya dunia matano kati ya 1914 na 1918 yaliyoonyeshwa kuwa yenye ukubwa wa 8 au zaidi kwenye skeli (kipimo) ya Richter—yenye nguvu zaidi ya lile tetemeko la dunia katika Abruzzi. Hata hivyo, mitikisiko hii ilikuwa katika maeneo ya mbali ya tufe, na hivyo hayakuvuta fikira sana kama lile tetemeko la Italia.5
-