-
Wale Wanawali Wenye Hekima na WapumbavuMnara wa Mlinzi—1990 | Aprili 15
-
-
Katika kielezi hicho, wale wanawali kumi hutoka na kwenda nje kwa kusudi la kukaribisha bwana-arusi na kujiunga katika mwandamano wa arusi. Awasilipo, wataangaza njia ya mwandamano kwa taa zao, hivyo kumheshimu aletapo bibi-arusi wake kwenye nyumba aliyotarishiwa. Hata hivyo, Yesu anaeleza hivi: “Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao; bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao. Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.”
-
-
Wale Wanawali Wenye Hekima na WapumbavuMnara wa Mlinzi—1990 | Aprili 15
-
-
Mafuta yafananisha kile kinachowaendeleza Wakristo wakiwa wanaangaza wakiwa vimulikaji, yaani, Neno la Mungu lililovuviwa, ambalo wanashika sana, pamoja na roho takatifu, ambayo husaidia katika kuelewa Neno hilo. Mafuta hayo ya kiroho huwezesha wale wanawali wenye busara waangaze nuru katika kumkaribisha bwana-arusi wakati wa mwandamano wa kwenda kwenye karamu ya arusi. Lakini jamii ya wale wanawali wapumbavu haina ndani yao, katika vyombo vyao, yale mafuta ya kiroho yanayohita-jiwa. Kwa hiyo Yesu aeleza linalotukia:
-