Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, ‘Utaendelea Kukesha’?
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
    • 9. (a) Yesu alitoa onyo gani kuhusu mwelekeo wa kulala usingizi? (b) Watiwa-mafuta wameitikiaje ule mwito: “Huyu hapa bwana-arusi!”? (Ona pia maelezo ya chini.)

      9 Sababu nyingine iliyowasaidia wale mabikira kuwa tayari ni kuwa macho. Je, Mkristo mtiwa-mafuta anaweza kusinzia anaposubiri kuja kwa Kristo? Bila shaka. Ona kwamba Yesu anasema hivi kuhusu wale mabikira kumi, “wote walisinzia na kuanza kulala” ilipoonekana kuwa bwana-arusi anachelewa. Yesu alijua kwamba hata mtu mwenye mtazamo wa kuendelea kukesha anaweza kudhoofishwa au kukengeushwa. Watiwa-mafuta waaminifu wametii onyo hilo na wamejitahidi hata zaidi kubaki macho na kukesha. Katika mfano huo, mabikira wote waliitikia mwito uliotolewa usiku: “Huyu hapa bwana-arusi!” Lakini mabikira waliokesha tu ndio waliovumilia hadi mwisho. (Mt. 25:5, 6; 26:41) Namna gani watiwa-mafuta waaminifu leo? Katika kipindi chote cha siku za mwisho, wameona uthibitisho ulio wazi ambao ni kana kwamba unatoa mwito huu, “Huyu hapa bwana-arusi!”—anakaribia kufika. Nao wameitikia mwito huo. Pia wamevumilia, na kuendelea kuwa tayari kabisa kwa ajili ya kuwasili kwa Bwana-arusi.a Hata hivyo, sehemu ya mwisho ya mfano huo inahusu kipindi hususa cha wakati. Jinsi gani?

  • Je, ‘Utaendelea Kukesha’?
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
    • a Katika mfano huo, muda fulani unapita kati ya kutolewa kwa ule mwito, “Huyu hapa bwana-arusi!” (mstari wa 6) na kuja au kuwasili kwa bwana-arusi (mstari wa 10). Katika kipindi chote cha siku za mwisho, watiwa-mafuta walio macho wametambua ishara ya kuwapo kwa Yesu. Kwa hiyo, wanajua kwamba Yesu yuko “hapa,” yaani, anatawala akiwa Mfalme. Hata hivyo, wanapaswa kuendelea kukesha hadi atakapokuja, au atakapowasili.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki