-
Je, ‘Utaendelea Kukesha’?Mnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
-
-
9. (a) Yesu alitoa onyo gani kuhusu mwelekeo wa kulala usingizi? (b) Watiwa-mafuta wameitikiaje ule mwito: “Huyu hapa bwana-arusi!”? (Ona pia maelezo ya chini.)
9 Sababu nyingine iliyowasaidia wale mabikira kuwa tayari ni kuwa macho. Je, Mkristo mtiwa-mafuta anaweza kusinzia anaposubiri kuja kwa Kristo? Bila shaka. Ona kwamba Yesu anasema hivi kuhusu wale mabikira kumi, “wote walisinzia na kuanza kulala” ilipoonekana kuwa bwana-arusi anachelewa. Yesu alijua kwamba hata mtu mwenye mtazamo wa kuendelea kukesha anaweza kudhoofishwa au kukengeushwa. Watiwa-mafuta waaminifu wametii onyo hilo na wamejitahidi hata zaidi kubaki macho na kukesha. Katika mfano huo, mabikira wote waliitikia mwito uliotolewa usiku: “Huyu hapa bwana-arusi!” Lakini mabikira waliokesha tu ndio waliovumilia hadi mwisho. (Mt. 25:5, 6; 26:41) Namna gani watiwa-mafuta waaminifu leo? Katika kipindi chote cha siku za mwisho, wameona uthibitisho ulio wazi ambao ni kana kwamba unatoa mwito huu, “Huyu hapa bwana-arusi!”—anakaribia kufika. Nao wameitikia mwito huo. Pia wamevumilia, na kuendelea kuwa tayari kabisa kwa ajili ya kuwasili kwa Bwana-arusi.a Hata hivyo, sehemu ya mwisho ya mfano huo inahusu kipindi hususa cha wakati. Jinsi gani?
-
-
Je, ‘Utaendelea Kukesha’?Mnara wa Mlinzi—2015 | Machi 15
-
-
a Katika mfano huo, muda fulani unapita kati ya kutolewa kwa ule mwito, “Huyu hapa bwana-arusi!” (mstari wa 6) na kuja au kuwasili kwa bwana-arusi (mstari wa 10). Katika kipindi chote cha siku za mwisho, watiwa-mafuta walio macho wametambua ishara ya kuwapo kwa Yesu. Kwa hiyo, wanajua kwamba Yesu yuko “hapa,” yaani, anatawala akiwa Mfalme. Hata hivyo, wanapaswa kuendelea kukesha hadi atakapokuja, au atakapowasili.
-