-
“Mtumwa Mwaminifu” na Baraza Linaloongoza LakeMnara wa Mlinzi—1990 | Machi 15
-
-
13 Katika kielezi kinacholingana na hicho, mfano wa talanta, Yesu alitaarifu kwamba baada ya muda mrefu, bwana-mkubwa alikuja kufanya hesabu na watumwa wake. Kwa wale watumwa waliothibitika kuwa waaminifu, bwana-mkubwa alisema hivi: “Ulikuwa mwaminifu juu ya machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.” Lakini kwa habari ya yule mtumwa asiye mwaminifu, alijulisha wazi hivi: “Hata kile alicho nacho atanyang’anywa. Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje.”—Mathayo 25:21-23, 29, 30.
14. Yesu alitarajia nini kwa watumwa wake wapakwa-mafuta?
14 Baada ya muda mrefu—karibu karne 19—Kristo alikabidhiwa mamlaka ya kifalme katika 1914, mwishoni mwa “nyakati zilizowekwa za mataifa.” (Luka 21:24, NW) Muda fupi baada ya hapo, ‘alikuja akafanya hesabu’ na watumwa wake, Wakristo waliopakwa mafuta kwa roho. (Mathayo 25:19) Kristo alitarajia nini kutoka kwao wakiwa mmoja mmoja na wakiwa jumla? Mgawo wa mtumishi-nyumbani uliendelea kama ulivyokuwa umekuwa tangu karne ya kwanza. Kristo alikuwa amewapa watu mmoja mmoja talanta—“kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake.” Hivyo, Yesu alitarajia matokeo ya kadiri. (Mathayo 25:15) Yenye kutumika hapa ni kanuni kwenye 1 Wakorintho 4:2, NW, ambayo hutaarifu hivi: “Kinachotazamiwa kwa watumishi-nyumbani ni mwanamume kupatikana mwaminifu.” Kufanyiza talanta kazi kulimaanisha kutenda kwa uaminifu kama “balozi” badala ya Kristo, kufanya wanafunzi na kuwagawia kweli za kiroho.—2 Wakorintho 5:20.
-
-
“Mtumwa Mwaminifu” na Baraza Linaloongoza LakeMnara wa Mlinzi—1990 | Machi 15
-
-
21. (a) Kristo alipata nani akigawanya chakula cha kiroho, na aliwathawabishaje? (b) Ni nini kilichongojea mtumwa mwaninifu na Baraza Linaloongoza lake?
21 Katika 1918, Kristo alipokagua wale waliodai kuwa watumwa wake katika 1918, alikuta kikundi cha kimataifa cha Wakristo kikitangaza kweli za Biblia kwa matumizi ndani ya kundi na nje pia katika kazi ya kuhubiri. Katika 1919 ikawa kweli kweli kama alivyokuwa ametabiri Kristo: “Mwenye furaha ni mtumwa yule ikiwa bwana-mkubwa wake wakati wa kuwasili amkuta akifanya hivyo. Kweli kweli mimi nasema kwenu nyinyi, Yeye atamweka juu ya mali zake zote.” (Mathayo 24:46, 47, NW) Hawa Wakristo wa kweli waliingia katika shangwe ya Bwana-Mkubwa wao. Wakiwa wamejionyesha kuwa ‘waaminifu juu ya vitu vichache,’ waliwekwa rasmi na Bwana-Mkubwa wawe ‘juu ya vitu vingi.’ (Mathayo 25:21) Mtumwa mwaminifu na Baraza Linaloongoza lake alikuwa katika mahali pake, tayari kwa mgawo uliopanuliwa. Yatupasa kuterema kama nini kwamba ilikuwa hivyo, kwa maana Wakristo wenye uaminifu-mshikamanifu wananufaika sana na kazi ya ujitoaji ya mtumwa mwaminifu na Baraza Linaloongoza lake!
-