-
“Mtumwa Mwaminifu” na Baraza Linaloongoza LakeMnara wa Mlinzi—1990 | Machi 15
-
-
13 Katika kielezi kinacholingana na hicho, mfano wa talanta, Yesu alitaarifu kwamba baada ya muda mrefu, bwana-mkubwa alikuja kufanya hesabu na watumwa wake. Kwa wale watumwa waliothibitika kuwa waaminifu, bwana-mkubwa alisema hivi: “Ulikuwa mwaminifu juu ya machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.” Lakini kwa habari ya yule mtumwa asiye mwaminifu, alijulisha wazi hivi: “Hata kile alicho nacho atanyang’anywa. Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje.”—Mathayo 25:21-23, 29, 30.
-
-
“Mtumwa Mwaminifu” na Baraza Linaloongoza LakeMnara wa Mlinzi—1990 | Machi 15
-
-
16. Kristo alipowasili kukagua nyumba ya Mungu katika 1918, kwa nini hakupata makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yakigawa chakula cha kiroho wakati ufaao?
16 Muda mrefu wa Yesu kungojea akiwa mkono wa kuume wa Yehova ulipokaribia kikomo, kidato kwa kidato ikaonekana wazi ni nani aliyekuwa akitoa chakula cha kiroho kwa watu wa nyumba ya Kristo hata katika wakati uliotangulia 1914. Je! unafikiri yalikuwa ni makanisa ya Jumuiya ya Wakristo? Bila shaka sivyo, kwa kuwa yalikuwa yamejihusisha sana katika siasa. Yalikuwa yamekuwa vyombo vyenye nia ya kutumiwa kupanua ukoloni na walikuwa wamejaribu kila mmoja kushinda mwingine ili kuthibitisha uzalendo wao, hivyo kutia moyo utukuzo wa taifa. Upesi hiyo ikawaletea hatia nzito ya damu, yaani, walipounga mkono kwa bidii serikali za kisiasa zilizohusika katika vita ya ulimwengu ya kwanza. Kiroho, imani yao ilikuwa imedhoofishwa na Umamboleo. Hali hatari ya kiroho ilitokea kwa sababu wengi wa makasisi wao walishawishwa kwa urahisi waamini uchambuzi wa juu na mageuzi. Hakuna chakula cha kiroho chenye kulisha ambacho kingetarajiwa kutoka kwa makasisi wa Jumuiya ya Wakristo!
17. Kwa nini Kristo aliwakataa Wakristo fulani wapakwa-mafuta, na matokeo yakawa nini kwao?
17 Vivyo hivyo, hakuna chakula cha kiroho chenye kulisha ambacho kingetarajiwa kutoka kwa wale Wakristo wapakwa-mafuta waliohangaikia zaidi wokovu wao wa kibinafsi kuliko kufanyiza kazi “talanta” ya Bwana-Mkubwa. Wakawa ‘walegevu,’ wasiofaa kuangalia mali ya Bwana-Mkubwa. Kwa hiyo, walitupwa ndani ya “giza la nje,” ambako makanisa ya Jumuiya ya Wakristo yangali yamo.—Mathayo 25:24-30.
-