Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
    • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kila Kikundi?

      16, 17. Kondoo watakuwa na wakati ujao gani?

      16 Yesu alitoa hukumu yake juu ya kondoo: “Njoni, nyinyi ambao mmebarikiwa na Baba yangu, rithini ufalme uliotayarishwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.” Huo ni mwaliko mchangamfu kama nini—“Njoni”! Wapate nini? Uhai udumuo milele, kama alivyoeleza katika umalizio wake: “Waadilifu [wataingia] katika uhai udumuo milele.”—Mathayo 25:34, 46, NW.

      17 Katika mfano wa talanta, Yesu alionyesha kile kinachohitajika kwa wale watakaotawala pamoja naye mbinguni, lakini katika mfano huu yeye aonyesha kile kinachotazamiwa kwa raia wa Ufalme. (Mathayo 25:14-23) Hasa, kwa sababu ya kuunga mkono kwa moyo wote ndugu za Yesu, kondoo watarithi sehemu katika makao ya kidunia ya Ufalme wake. Wao watafurahia uhai katika dunia iliyo paradiso—tazamio ambalo Mungu aliwatayarishia “tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu” wa wanadamu wawezao kukombolewa.—Luka 11:50, 51, NW.

  • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
    • 19 Wanafunzi wa Biblia wajua kwamba hilo haliwezi kumaanisha kwamba nafsi zisizoweza kufa za wenye mfano wa mbuzi zitateseka katika moto wa milele. La, kwa kuwa wanadamu ni nafsi; hawana nafsi zisizoweza kufa. (Mwanzo 2:7; Mhubiri 9:5, 10; Ezekieli 18:4) Kwa kuhukumu mbuzi kwa “moto wa milele,” Hakimu anamaanisha uharibifu usio na tumaini la wakati ujao, ambao pia utakuwa mwisho wa daima wa Ibilisi na roho waovu wake. (Ufunuo 20:10, 14) Hivyo, Hakimu wa Yehova atoa hukumu hizo zilizo tofauti. Awaambia kondoo, “Njoni”; mbuzi, “Ondokeni kwangu.” Kondoo watarithi “uhai udumuo milele.” Mbuzi watapatwa na “kukatiliwa-mbali kudumuko milele.”—Mathayo 25:46, NW.b

  • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
    • 21 Hata hivyo, uelewevu huu mpya wa mfano wa kondoo na mbuzi wamaanisha nini kwetu? Naam, tayari watu wanachukua misimamo. Wengine wamo katika ‘barabara pana iongozayo katika uharibifu,’ huku wengine wakijaribu kudumu katika ‘barabara yenye kufinyana iongozayo katika uhai.’ (Mathayo 7:13, 14, NW) Lakini wakati ambapo Yesu atatangaza hukumu ya mwisho juu ya kondoo na mbuzi wanaoonyeshwa katika huu mfano ungali mbele. Mwana wa binadamu ajapo katika fungu la Hakimu, yeye ataamua kwamba Wakristo wengi wa kweli—hasa “umati mkubwa” wa kondoo waliojiweka wakfu—watastahili kupita sehemu ya mwisho ya “dhiki kubwa” na kuingia katika ulimwengu mpya. Tazamio hilo lapaswa sasa kuwa chanzo cha shangwe. (Ufunuo 7:9, 14, NW) Kwa upande mwingine, halaiki ya watu kutoka kwa “mataifa yote” watakuwa wamejithibitisha kuwa mbuzi washupavu. Wao “[wataingia] katika kukatiliwa-mbali kudumuko milele.” Liwazo lililoje kwa dunia!

  • Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?
    Mnara wa Mlinzi—1995 | Oktoba 15
    • b El Evangelio de Mateo chaeleza: “Uhai udumuo milele ni uhai wa hakika; kinyume chao ni adhabu ya hakika. Kivumishi cha Kigiriki aionios hasa hakionyeshi kipindi cha wakati, bali hali. Adhabu ya hakika ni kifo cha milele.”—Profesa mstaafu Juan Mateos (Pontifical Biblical Institute, Rome) na Profesa Fernando Camacho (Kituo cha Kitheolojia, Seville), Madrid, Hispania, 1981.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki