Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wanaume Watatu Wenye Hekima” Walikuwa Nani? Je, Walifuata “Nyota” ya Bethlehemu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
    • Mchoro unaoonyesha wanaume watatu wenye hekima wakimletea mtoto Yesu zawadi

      “Wanaume Watatu Wenye Hekima” Walikuwa Nani? Je, Walifuata “Nyota” ya Bethlehemu?

      Jibu la Biblia

      Tofauti na desturi maarufu inayohusisha Krismasi, Biblia haitumii maneno “wanaume watatu wenye hekima” au “wafalme watatu” inapozungumzia wasafiri walioenda kumtembelea Yesu alipozaliwa. (Mathayo 2:1) Badala yake mwandishi wa Injili Mathayo alitumia neno la Kigiriki ma’goi kuwazungumzia wale waliomtembelea Yesu. Huenda neno hilo linarejelea wataalamu wa unajimu na mambo mengine ya kichawi.a Baadhi ya tafsiri za Biblia huwaita “wanajimu” au “mamajusi.”b

  • “Wanaume Watatu Wenye Hekima” Walikuwa Nani? Je, Walifuata “Nyota” ya Bethlehemu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
    • “Wanaume wenye hekima” walikuwa Wangapi?

      Biblia haitaji idadi na kulingana na desturi mbalimbali idadi hiyo inatofautiana. Encyclopedia Britannica inasema, “Kulingana na desturi za Mashariki idadi ya Mamajusi ilikuwa 12, na watatu kulingana na desturi za Magharibi, labda kwa sababu ya zawadi walizompa mtoto, yaani ‘dhahabu, ubani na manemane’ (Mathayo 2:11).”

      Je “wanaume wenye hekima” walikuwa wafalme?

      Ingawa katika desturi ya Krismasi wageni hao wanaonyeshwa kwa njia hiyo, hakuna sehemu yoyote ya Biblia inayowaita wafalme. Kulingana na Encyclopedia Britannica, cheo hicho kiliongezwa baada ya karne kadhaa kama sehemu ya desturi “zilizotia chumvi masimulizi hayo.”

      Je, majina ya wale “wanaume wenye hekima” yanajulikana?

      Biblia haifunui majina ya wanajimu hao. Kulingana na kitabu The International Standard Bible Encyclopedia, “majaribio ya kuwapa majina (kama vile, Gaspar, Melchior, na Balthasar) yanategemea hekaya.”

  • “Wanaume Watatu Wenye Hekima” Walikuwa Nani? Je, Walifuata “Nyota” ya Bethlehemu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
    • a Herodoto, mwanahistoria Mgiriki wa karne ya tano K.W.K., alisema kwamba ma’goi wa wakati huo walikuwa wa kabila fulani la Wamedi (Waajemi) ambalo lilizoea kufanya unajimu na kufasiri ndoto.

      b Ona New American Standard Bible, The New American Bible, The New English Bible, na New International Version Study Bible. Tafsiri ya King James inarejelea wageni hao kama “watu wenye hekima,” lakini haisemi kwamba walikuwa watatu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki