Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 12/15 uku. 30
  • Je, Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Unaweza Kumpata Ndugu Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Mungu Aliye “Tayari Kusamehe”
    Mkaribie Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 12/15 uku. 30

Je, Wakumbuka?

Je, umeyafikiria kwa makini matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, utapendezwa kukumbuka yafuatayo:

◻ Wakristo wawili wanaweza kujiuliza maswali gani kabla ya kuanza kufikiria uchumba?

‘Je, kweli naijua vema hali ya kiroho ya mtu huyo na ujitoaji wake kwa Mungu? Je, naweza kutazamia kumtumikia Mungu maisha yote nikiwa naye? Je, tunafahamu vema tabia za kila mmoja? Je, nina uhakika kwamba tutaendelea kupatana daima? Je, twafahamu mambo ya kutosha juu ya matendo ya wakati uliopita na hali za sasa za kila mmoja?’—8/15, ukurasa wa 31.

◻ Yesu alimaanisha nini alipowaambia wafuasi wake: “Nyinyi ndio chumvi ya dunia”? (Mathayo 5:13)

Yesu alidokeza kwamba mahubiri ya wanafunzi wake juu ya Ufalme wa Mungu yangekuwa na uvutano uwezao kuhifadhi au kuokoa uhai kwa wanaosikiliza. Kwa kweli wale waliotumia maneno ya Yesu wangelindwa wasipatwe na uozo wa kiadili na wa kiroho ulio katika ulimwengu.—8/15, ukurasa wa 32.

◻ Watu wanaochumbiana wanaweza kuepukaje mtego wa ukosefu wa adili kingono?

Ikiwa una mchumba, ni jambo la busara kuepuka kuwa peke yako na yule atakayekuwa mwenzi wako katika hali zisizofaa. Kwa hiyo, huenda ikawa bora zaidi kufurahia ushirika wenu mkiwa katika kikundi au mahali pa umma. Wekeni mipaka kuhusu kuonyeshana shauku, kila mmoja akiheshimu hisia na dhamiri ya mwenziwe.—9/1, ukurasa wa 17, 18.

◻ Uelewevu ni nini?

Huo ni uwezo wa kuchunguza jambo na kupambanua muundo wake kwa kujua uhusiano kati ya sehemu zake mbalimbali na kati ya muundo wake mzima, hivyo kulielewa. (Mithali 4:1)—9/15, ukurasa wa 13.

◻ Yehova hutaka nini kutoka kwetu leo?

Kwa ujumla, Yehova hutaka tumsikilize Mwana Wake na kufuata kielelezo chake na mafundisho yake. (Mathayo 16:24; 1 Petro 2:21)—9/15, ukurasa wa 22.

◻ Ni nani pekee wawezao kupata amani?

Kwa kuwa Yehova ndiye “Mungu apaye amani,” wale wanaompenda Mungu na kustahi sana kanuni zake za uadilifu ndio watu pekee wawezao kupata amani. (Waroma 15:33)—10/1, ukurasa wa 11.

◻ Yosefu alipataje nguvu za maadili za kumkataa mke wa Potifa siku baada ya siku?

Yosefu alithamini sana uhusiano wake pamoja na Yehova kuliko alivyothamini raha za muda tu. Isitoshe, ingawa hakuwa chini ya sheria ya Mungu, Yosefu alifahamu kabisa kanuni za maadili. (Mwanzo 39:9)—10/1, ukurasa wa 29.

◻ Utayari wetu wa kuwasamehe ndugu zetu ni muhimu kadiri gani?

Kuendelea kupokea msamaha wa Mungu kwategemea sana utayari wetu wa kuwasamehe wengine. (Mathayo 6:12, 14; Luka 11:4)—10/15, ukurasa wa 17.

◻ Andiko la Mathayo 18:15-17 larejezea dhambi za aina gani, na ni jambo gani linaloonyesha hivyo?

Dhambi ambazo Yesu alimaanisha zilikuwa nzito kiasi cha kwamba zingeweza kufanya mkosaji aonwe “kama vile mtu wa mataifa na kama mkusanya-kodi.” Wayahudi hawakuwa na shughuli na watu wasio Wayahudi, na waliwaepuka wakusanya-kodi. Basi andiko la Mathayo 18:15-17 larejezea dhambi nzito, si kuumizwa au makosa madogo-madogo ya kibinafsi ambayo unaweza kusamehe tu na kusahau. (Mathayo 18:21, 22)—10/15, ukurasa wa 19.

◻ Kupenda Neno la Mungu kwelikweli kwahusisha nini?

Kupenda Neno la Mungu humfanya mtu aishi kupatana na matakwa ya Mungu. (Zaburi 119:97, 101, 105) Hilo lahitaji mtu arekebishe daima fikira zake na maisha yake.—11/1, ukurasa wa 14.

◻ Tukiwa tumepokea vitu vingi sana kutoka kwa Yehova, twaweza kumpa nini huyu Mfalme na Mpaji mkuu zaidi?

Biblia hufunua kwamba zawadi iliyo bora zaidi tuwezayo kumpa Yehova ni “dhabihu ya sifa.” (Waebrania 13:15) Kwa nini? Kwa sababu dhabihu hiyo inahusiana moja kwa moja na kuokoa uhai, jambo ambalo Yehova anahangaikia zaidi wakati huu wa mwisho. (Ezekieli 18:23)—11/1, ukurasa wa 21.

◻ Solomoni alimaanisha nini alipoandika: “Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoro”? (Mhubiri 12:11)

Maneno ya wale wenye hekima ya kimungu huwachochea wasomaji au wasikilizaji wafanye maendeleo kwa kupatana na maneno yenye hekima yanayosomwa au kusikizwa.—11/15, ukurasa wa 21.

◻ Ufahamu wa kimungu ni nini?

Ufahamu wa kimungu ni uwezo wa kupambanua mema na mabaya, kisha kuchagua mwenendo ufaao. Kujifunza na kutumia Neno la Mungu hutupa ufahamu.—11/15, ukurasa wa 25.

◻ Utayari wa kukubali madaraka wahitaji kusawazishwa na nini? (1 Timotheo 3:1)

Huo wapaswa kusawazishwa na maamuzi yafaayo. Mtu yeyote asikubali migawo mingi sana hivi kwamba anapoteza furaha yake katika utumishi wa Yehova. Ndiyo, ni vizuri kuwa na roho ya utayari, lakini utayari huo wapaswa pia uwe na kiasi na “utimamu wa akili.” (Tito 2:12; Ufunuo 3:15, 16)—12/1, ukurasa wa 28.

◻ Wazazi wanaweza kukabilije ugumu wa kulea watoto?

Mungu huwashauri wazazi wawe vielelezo, rafiki, wawasilianaji, na walimu. (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7)—12/1, ukurasa wa 32.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki